Sunday 7 July 2013

MANDELA ATEMBELEWA NA MFUNGWA MWENZAKE

Denis Goldberg ambaye kwa sasa ana miaka 80

Denis Goldberg (mwanaharakati mweupe) alikuwa hospitalini alikolazwa Mandela Jumatatu iliyopita alipokwenda kumtembelea.

Rafiki mmoja wa karibu wa Nelson Mandela jana alidai kwamba rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini anayeumwa alikuwa 'mwenye fahamu zake kamili' wakati alipomtembelea hospitalini wiki hii.

Denis Goldberg, mwanaharakati mweupe wa kupinga ubaguzi wa rangi na mfuasi wa chama tawala cha African National Congress (ANC), alihitilafiana na maoni ya kitabibu yaliyowasilishwa mahakamani wiki hii, ambayo yanaeleza kwamba Mandela amekuwa kwenye 'hali ya kulala tu' kwa siku tisa zilizopita na familia yake ilikuwa ikijadiliana kuhusu kuzima mashine zake za kuokolea maisha.Ripoti hizo za kitabibu juu ya hali ya Mandela zimeibuka wakati wa kesi ya mahakamani wiki hii kati ya wanafamilia ya Mandela wanaovutana wakigombea kuhusu wapi atakapozikwa mshindi huyo wa Tuzo ya Amani ya Nobel.


Goldberg, ambaye alifungwa jela kwa miaka 22 wakati wa mashitaka maarufu ya Rivonia ya mwaka 1964 ambayo yalishuhudia Mandela akihukumiwa kifungo cha maisha, alisisitiza kwamba alimtembelea Mandela Jumatatu na kwamba alimwona 'dhahiri ni mtu anayeumwa sana, lakini alizisikia sauti na kujaribu kuongea."

Aliongeza: "Alikuwa amelala fofofo wakati nilipoingia pale. Nilizungumza na kumweleza mimi ni nani na akafungua macho yake na kunitazama. Niliongea naye kwa takribani dakika kumi na alionesha kuelewa nilichokuwa nikiongea. Alinitambua mimi ni nani."

Goldberg, ambaye alitumikia hukumu yake kwenye gereza la wazungu mjini Pretoria wakati Mandela alisafirishwa kwa meli kwenda Kisiwa cha Robben, alisema Mandela mwenye miaka 94 'alikuwa hana nguvu lakini alikuwa mwenye fahamu zake kamili."

Aliongeza: "Hakuweza kujibu sababu hawezi kuongea, akiwa na mipira kwenye koo lake, lakini alikuwa akitingisha taya lake kana kwamba anataka kuongea. Hakika nilishangaa sana - baada ya taarifa nilizokuwa nimezisikia."

Huku wengi wa watu wa Afrika Kusini wamekata tamaa kwenye ukweli kwamba Mandela hawezi kupona, taarifa zinazokinzana kuhusu afya yake zimesababisha hofu kuu, huku mmoja wa watangazaji akiishutumu serikali ya ANC kwa kupotosha umma.

CHANZO: Vijimambo

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...