Saturday 27 July 2013

UDAKU MWINGINE JAMANI: LULU AZUA HEKAHEKA

Stori:Denis Mtima
MWIGIZAJI mahiri Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ Jumatano iliyopita alizua hekaheka mtaani baada ya kutinga kwenye duka moja na watu kumtumbulia macho kwa kumshangaa.

Tukio hilo lilitokea kwenye duka hilo lililopo Sinza Afrika Sana ambapo staa huyo mwenye kesi ya madai ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa staa wa filamu za Bongo, marehemu Steven Kanumba, alitinga dukani hapo akihitaji huduma ya fedha kwa njia ya mtandao wa simu.
Baadhi ya watu waliokuwa wanapita jirani, walimkodolea macho Lulu huku kila mtu akisema lake. Mtu mmoja ambaye hakutambulika jina, alisikika akisema:
“Ametulia siku hizi, tangu ametoka Segerea amekuwa mtulivu sana.”
Baada ya kuhudumiwa, Lulu alitoka lakini baadaye akagundua kuwa amesahau funguo ya gari, hali iliyomlazimu kurudi dukani.
Aliporudi dukani, aliiona funguo hiyo, akatoka na kwenda kwenye gari alilokuja nalo. Ndani ya gari hilo aina ya Toyota Mark II, alikuwa na mdogo wake ambaye jina lake halikupatikana mara moja.

CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...