Monday 1 July 2013

Wasanii wa Tamasha la Filamu Grand Malt watoa msaada wa vyandarua hospitali ya Sekou-toure leo jijini mwanza


 Picha ya pamoja na viongozi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza.
 Sehemu ya vyandarua vilivyotolewa msaada vikiwa tayari vimefungwa na wasanii wa filamu hapa nchini,mara baada ya kutoa msaada wa vyandarua hivyo ndani ya wodi ya wazazi kwenye hospitali ya Mkoa wa jiji la Mwanza-Sekou-toure  mapema leo asubuhi kwa udhamini mkubwa wa kinywaji kisicho na kilevi cha Grandmalt..
 Msanii wa Bongo Movie,Jacline Wolper akiwa katika wodi ya wazazi ,Hospital ya Mkoa wa Mwanza Sekou-toure akifunga chandarua kwenye moja ya vitanda hospitalini hapo,ikiwa ni sehemu ya vyandarua vilivyotolewa na wasanii hao kupitia kinywaji cha Grandmalt
 Wasanii Irine Uwoya na Shamsa Ford wakiwa na mmoja wazazi akiwa amembeba mtoto aliezaliwa kwenye hospitali hiyo ya Mkoa wa Mwanza, Sekou-toure  mara baada ya wasanii hao kutembelea Hospitali hiyo na kutoa vyandarua kwenye wodi Wazazi.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Mwanza,Halifa Hassan Hida akizungumza machache (mbele ya wasanii wa Bongo Movie (hawapo pichani) ikiwemo na kuwashukuru wasanii hao wa filamu kwa kitendo cha kiungwana kabisa katika suala zima la kuisaidia jamii yao inayowazunguka kwa njia moja ama nyingine na pia amewataka kuwasaidia wasanii wachanga wa jiji la Mwanza na kuwaelekeza njia sahihi za mafanikio katika tasnia hiyo ambayo kwa sasa imezidi kushika kasi siku siku. 


 Meneja wa kinywaji cha Grandmalt Consolata Adam akipokea mkono wa shukurani  kutoka kwa katibu wa Afya hospitali ya Sekou-toure Bwa.Daniel Temba,mara baada ya kabidhi msaada wa vyandarua sanjari na wasanii mbalimbali wa filamu,makabidhiano hayo yamefanyika mapema leo kwenye hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekou-toure,ikiwa ni sehemu ya wasanii hao kuwa karibu na wananchi, kisha baadae kuonyesha kazi zao mbalimbali kwenye uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.
Wasanii mbalimbali wakiongozwa na Raymond Kigosi  wakikabidhi msaada wa vyandarua kwenye hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekou-toure, kwa katibu wa afya wa Hospitali  hiyo Bwa.Daniel Temba ikiwa ni sehemu ya wasanii hao kuwa karibu na wananchi, kisha baadae kuonyesha kazi zao mbalimbali kwenye uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.
 wasanii wakiendelea na zoezi la  wakikabidhi msaada wa vyandarua kwenye hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekou-toure kwa katibu wa afya wa Hospitali  hiyo ikiwa ni sehemu ya wasanii hao kuwa karibu na wananchi, kisha baadae kuonyesha kazi zao mbalimbali kwenye  uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza.
 Baadhi ya wasanii wa Filamu hapa nchini a.k.a Bongo Movie Unity wakiwasili kwenye hospitali ya Sekou-toure tayari kwa kushiriki zoezi la kugawa vyandarua kwenye wodi ya wazazi kwa udhamini mkubwa wa kinywaji kisicho na kilevi cha GrandMalt mapema leo asubuhi.
 Mlezi wa Bongo Movie Unity,Jacob Steven a.k.a JB a.k.a Bonge la Bwana wakisalimiana na Afisa mhausiano wa Halmashauri ya jiji la Mwanza,Bwa.Joseph Mlinzi,pichani kati ni msanii wa filamu Singo Mtambalike.
 Baadhi ya Wasanii hao wa Bongo Movie Unit wakitoka kwenye wodi ya Wazazi mara baada ya kukabidhi msaada wa vyandarua vilivyotolewa kwa hisani kubwa ya kinywaji kisicho na kilevi cha Grandmalt

CHANZO:Mtaa kwa mtaa

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...