Saturday 28 February 2015
GAUNI LENYE SHANGA ZA LULU LA LUPITA NYONGO LILILOIBWA, LAPATIKANA
Hatimae
gauni la muigizaji wa kike Lupita
Nyongo,lililoibwa kutoka katika hoteli aliyokuwa akikaa,limepatikana. Gauni
hilo lililotengenezwa kwa shanga za lulu alilivaa katika tuzo za Oscar.
THE GARDEN: JE,UNAYAFAHAMU MATUNDA HAYA?
Ninayatamani
sana matunda haya ambayo wakati wa utoto wangu nimeyala sana.Kwa wale wa Dar es
salaam,yanapatikana wapi? Niliyajua kwa majina ya topetope au stafeli.Je,wewe
mdau, unayajua kwa majina gani?
Friday 27 February 2015
Thursday 26 February 2015
Wednesday 25 February 2015
DESIGN ZA NYUMBA NA PLAN ZAKE KWA WALE WANAOTAKA KUMILIKI MIJENGO
Plan ya nyumba 2 ambazo kidogo zinafanana, tofauti moja
ina gereji ya gari nyingine haina na tofauti nyingine ni mpishano wa sehemu ya kufulia na store. Chagua kulingana
na matakwa yako.
Tuesday 24 February 2015
Monday 23 February 2015
TUSEME BASI KWA MAUAJI YA ALBINO
TUSEME BASI KWA MAUAJI YA ALBINO!
Ninashindwa kuelewa nianzie wapi kuandika hii makala ya leo.Maana
ninaandika mikono ikitetemeka kwa kweli. Nashindwa kuelewa hasa lawama zangu
nizielekeze kwa nani. Sijui kama ni kwa serikali au wananchi,ama kwa wote.
Hivi ni kweli tumeshindwa kuwalinda watu wenye ulemavu wa ngozi?
Hawa watu wenye ulemavu wa ngozi wanaishi wapi na wanao waua kikatili nao
wanaishi wapi? Je,wanaishi katika nchi tofauti au sayari tofauti? Kama la, je
ni kweli jamii inayoishi katika maeneo husika haijui ni nani wanaotenda vitendo
hivyo? Kama wanajua kwanini wanakaa kimya?
Friday 20 February 2015
THE GARDEN: PALM TREE INAVYOWEZA KUPENDEZESHA MAZINGIRA YA NYUMBA YAKO
Kuna aina nyingi ya mimea unayoweza
kuweka katika bustani yako ya maua.Katika bustani zetu za maua sisi wote huweka
mimea ambayo ni chaguo letu. Katika mimea niipendao Palm, na fern ni miongoni mwa hiyo
mimea.Je,wewe msomaji unapenda ipi?
Tuangalie baadhi ya palm na fern zikiwa
zimepandwa kwa kuchanganywa na mimea mingine kiubunifu ili kuleta mvuto
unaotakiwa katika bustani yako.
Palm tree na fern zilivyopendeza
hapa
Subscribe to:
Posts (Atom)
PALM TREES ARE BEAUTIFUL
Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...
-
Dar es Salaam: Mwekezaji Sheikh Salim Abdullah ametangaza kuwekeza kwenye Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere Dar es Salaam (JN...