Thursday 24 December 2015

MERRY CHRISTMAS KWENU WOTE!!




Rainbow-tz blog inawatakia wote heri ya sikukuu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo,maarufu kama KRISMASI. Katika kusherehekea sikukuu hii tulete upendo pale palipo na chuki na hekima pale palipojaa dharau.Kwa mliojaliwa kidogo mkumbuke kuwa kuna waliokosa kabisa hivyo tuwakumbuke nao katika hicho kidogo.Usitupe chakula wakati jirani yako ananjaa, usitupe nguo wakati jirani yako yupo uchi na usimwage maji wakati jirani yako ana kiu.
Mungu awabariki wote .

MERRY CHRISTMAS!!

Tuesday 15 December 2015

Sunday 13 December 2015

THE WARDROBE :AFRICAN PRINT DESIGNS

African print hupendeza zaidi inaposhonwa kibunifu na si kuweka urembo mwingi.Angalia mitindo ifuatayo kuthibitisha hilo.

KALI YA SIKU

USHAURI JUU YA KUOA

1: Usioe kwa sababu umechoka kula kwa mama lishe>>Mke sio mpishi kama umechoka kula kwa mama lishe jifunze kupika.

2: Usioe kwa sababu umechoka kufua na kupika >>Mke sio housemaid, kama umechoka kufua ajiri mtu akufulie.

3: Usioe kwa sababu rafiki zako wote wameoa >>Mke sio mashindano maana hataishi na marafiki zako wala sio zawadi kwa wazazi wako bali wewe ndiwe utakayeishi naye.

4: Usioe kwa sababu unataka kufungua kanisa sasa unatafuta mama mchungaji

5: Usioe kwa sababu wazazi wanakulazimisha maana dada zako wote wameshaolewa.

6: Usioe kwa sababu mpenzi au mchumba amepata mimba yako.

7: Usioe kwa sababu unataka kumuonyesha msichana aliyekuacha kuwa bado upo juu.

8: Usioe kwa sababu unamhurumia msichana uliyenaye ukimuacha atachanganyikiwa.

9: Usioe kwa sababu wazazi wako wanampenda na kumkubali msichana huyo.

10: Kuliko kumuoa msichana kwa kumhurumia na si kumpenda itapelekea kuteseka moyoni maisha yenu yote ni afadhali umwambie ukweli kungali mapema

11: Kuoa ili kujionyesha kuwa ume-move on baada ya kuachwa ni kujikomoa mwenyewe.

Oa ukiwa na uhakika kuwa huyo ndiye chaguo lako pekee na upo tayari kuishi naye katika hali zote, ndio mpango wa Mungu katika maisha yako na ndiye unayempenda kwa moyo wako wote.

Diamond Platnumz - Utanipenda

Friday 11 December 2015

UJUMBE KWA MWANANGU

Mwanangu MPENDWA, naomba unisikilize kwa uzuri kabla HUJAOA.
1. Mwanangu, mwanamke anaweza kuwa mkeo, mwingine anaweza kuwa mama wa watoto wako, lakini ukipata mwanamke ambae atakuwa kama mama kwako, mama kwa wanao na mama kwa familia, tafadhari mwanangu usimuache huyo!
2. Mwanangu, usimfanye mwanamke wako kuwa ndio wa kupika na kufanya kazi zote za jikoni peke yake, tabia hiyo sio nzuri kwani hata nyakati zetu, mashamba yetu yalijulikana kwa majina yetu wanaume lakini tulifanya kazi pamoja!
3. Mwanangu, nikikwambia wewe ni kichwa cha familia, simaanishi kutuna kwa pochi lako, usiangalie kabisa pochi yako, angalia kama utaona tabasamu usoni kwa mke wako. Pesa sio kila kitu katika ndoa na haileti ukuu wa familia!
4. Mwanangu, ukitaka kuwa na maisha marefu na ukapunguza misongo ya mawazo, ongea na mkeo pangeni bajeti ya mahitaji yenu pamoja, kisha mwache mkeo awe na jukumu la kuratibu mahitaji ya kila siku ya familia kwa kumkabidhi fungu husika hata kama limetokana na michango yenu wawili. wanawake wanajua sana kupanga bajeti na hii haitakuwa rahisi kwa yeye kutumia hela hovyo wakati akijua kuwa nyumbani kuna mahitaji ya msingi, lakini hela zikiwa mikononi mwako ataendelea kuomba hata kama utakuwa umeishiwa!

Wednesday 9 December 2015

MY HUSBAND'S FAMILY DOES NOT LIKE ME

Marriage comes with a lot of issues these days especially when one isn’t from the same tribe with the spouse. Tolani is from the west while Solomon is from the middle-belt. Tolani family members are in full support of their affair but Solomon family are not in support. Before they tied the knot a lot happened but they weren’t discourage. Solomon was so in love with his wife that he stoped her from attending his family gatherings.

PICHA:RAIS JOHN POMBE MAGUFULI AONGOZA ZOEZI LA USAFI

Katika kuadhimisha miaka 54 ya uhuru,rais  John Pombe Magufuli  ameshtaki katika zoezi la usafi JIJINI Dar es salaam.
Chini ni picha zikimuonyesha akiwa katika zoezi hilo.

Tuesday 8 December 2015

Koffi Olomide - Selfie

JIHADHARI NA NDUMILAKUWILI

Ni mtu/rafiki anaye jifanya mwema na kukupenda mkiwa pamoja, ukipa mgongo anakusema vibaya kwa watu na kufanya jambo lolote ili akuharibie. Ndumila kuwili siku zote wanakuwa ni watu wa karibu marafiki, jirani, ndugu, mfanyakazi mwenzio, ndio maana hata siku moja hukai ukawaza anaweza kuja kukutenda. Kitu kikubwa chukua tahadhari mapema;

Kaa mbali na mtu anayependa kuhadithia au kutoa siri za watu wengine, ujue siku akija kujua na ya kwako ataenda tu kuyatangaza. Na ukiwa unapenda kumsikiliza mtu mmbea, anaweza hata kukugeuzia kibao kwa watu kuwa umewasema wakati yeye ndiye aliyesema.

Usipende kuongea mambo yako kwa kila mtu, hata kama ni mafanikio, ujue ndumila kuwili wengi wana chuki, wivu hawapendi kuona wengine wana fanikiwa, akijua mambo yako yanaenda vizuri atafanya kila analo weza uharibikiwe iwe kazini, ndoa, heshima yako kwa watu nk.

Ndumila kuwili akishakutenda usipende kumwamini tena, mwingine anaweza kupamba msamaha lakini moyoni hajamaanisha, rafiki unaweza kununua urafiki ila mwingine ni nduguyo, mfanyakazi mwenzio lazima kuna mahala utakutana naye, ila kwa vile nyoka umeshamjua unachukua tahadhari mapema.

Ndumila kuwili akishakutenda mpe ukweli wake, uguza maumivu mwombe Mungu akusaide endelea na maisha yako, haina haja kukaa unaendelea kumtumia meseji au kumpigia simu mnatukanana mpaka kwenye mitandao , inauma ndio lakini muhimu ushajifunza na yaliyotokea.

Monday 7 December 2015

WALIOTOKELEZEA

ROBERT MUGABES'S LETTER TO WHITE MEN


Dear white men, U asked us to wear coats under hot sun,
we did;
~
U said we should speak your language, we have obediently
ignored ours.
~
U asked us to always tie a rope around our necks like goats,
we have obeyed without questioning.
~
U asked our ladies to wear dead people's hair instead of the
natural hair God gave to them, they have obeyed.

Sunday 6 December 2015

BINTI ALIYEWALIZA WENGI BAADA YA KIFO CHAKE-INAUMIZA SANA


Baada ya mahusiano ya zaidi ya miaka mitatu na siku kadhaa kijana alishindwa kuhimili shinikizo la ndugu na kumwacha mpenzi wake kwa madai kuwa sio wa hadhi yake. Akapewa mke mpya na baadae kuanza maisha mpya na ndugu wakifurahia uamuzi wao wa kumpa kijana wao mke mpya huku wakimsahau yule dada wa kwanza.

Binti yule wa kwanza akaondoka na kwenda mji mwingine kuanza maisha yake huku akijikita katika biashara zake.
Siku zikapita na kila mtu akasahau mkasa ule wa binti aliyefukuzwa kabla ya kijana kuanza kuumwa.

Wakazunguka kila hospitali bila kupata tiba mpaka pale walipokuja kugundua kuwa figo zake zimeharibika na hawezi tena kupona kama sio kupata figo kutoka kwa mtu wa karibu au afe.

Ndugu na marafiki wakamkwepa na kumwacha akiwa kalala pale hospital bila ya msaada na kila mmoja akiogopa kutoa figo kumpa kijana apone na mbaya zaidi hata mke wake mpya akawa amekimbia na kurudi kwao.

Mama wa kijana alizidi kumtunza kijana akiwa hana namna ya kumsaidia kwani kwa uzee ule alikataliwa kutoa figo yake imsaidie mwanae apone.
Siku zikasogea na yule mchumba wa kwanza aliyefukuzwa akapata habari za mpenzi wake wa mwanzo kuwa hali sio nzuri. Kwa huruma akaja mpaka hospitalini na kukubali afanyiwe upasuji na atolewe figo moja.

Kabla ya upasuaji aliomba karatasi na kuandika kitu na kumpa daktari amwekee. Kwa bahati mbaya baada ya upasuaji yule dada alifariki na kijana baada ya wiki kadhaa alipona na kuwa mzima kabisa.

Siku moja akaenda hospitali ili amshukuru daktari na wote waliomsaidia akiwa pale hospitali, akiwa chumbani kwa daktari alipokea karatasi kutoka kwa dakatari na kuambiwa kuna mtu aliyemsaidia kutoa figo kabla hajafa alimwachia karatasi... Kaka kabla ya kusoma akaumia sana na kusema laiti mtu huyo angekuwa mzima amshukuru kwa moyo ule wa huruma na kisha akaifungua ile karatasi na iliandikwa:-

"Mpenzi wangu Nolesy kama unausoma ujumbe huu basi ujue wewe ni mzima na umepona sasa baada ya mimi kukupa figo yangu.

Nilikupa moyo wangu ukauumiza sana na kunipa majeraha makali huku ukinitazama bila huruma.

Sasa nimekupa figo yangu, naomba uipende sana hata kama hautaniona mimi kama ilivyokuwa kwa moyo wangu.

Nakutakia maisha mema.

Zilipendwa wako Habiba"

Siku moja baada ya kuusoma ule ujumbe kijana yule siku ya tatu yake alikutwa amekufa kwa kujinyonga.

Rafiki shikilia ulichonacho sasa kwa maana ni baraka kwako na huwezi ona umuhimu wake mpaka utakapokipoteza au kukikosa kabisa.
Utakuwa na furaha ya muda mfupi  sana ila utateseka maisha yako yote.
Siku zote Mungu hulipa kwa namna yake.
Tusisahau utu kwa tamaa zetu za mwili.

Saturday 5 December 2015

NENO LA LEO


UJINGA HAUNA MWALIMU!

KALI YA SIKU

MKE WA KUOA

Ukitaka majungu oa Mhaya,
Ukitaka mapenzi ya ujanja ujanja na uwizi wa mfukoni oa Mchaga,
Ukitaka uchawi oa Mfipa,
Ukitaka maneno oa Mzenji,
Ukitaka mapishi oa Mtanga,
Ukitaka mume mwenza oa Mzaramo,
Ukiwa na shamba oa Msukuma,
Ukitaka mapenzi ya kuona aibu oa Mhehe,
Ukitaka kubana matumizi oa Mpare,
Ukitaka kisukari oa Mwarabu mara tende mara halua,
Ukitaka kujichanganya oa Mkerewe au Mjita,
Na kama unataka kuwachanganya mtu na dada yake oa Mrangi,
Ukitaka kubishana oa Mnyirmba
Ukitaka kupigana oa Mkuryaa,
Ukitaka kuzaa sana oa Muha,
Ukitaka kubembelezwa na kudanganywa oa Mnyamwezi
Ukitaka Mke anayejali watu na kulala kwenye misiba oa Mnyakyusa.

Wednesday 2 December 2015

KILA KIUMBE WA KIKE- CHRIS MAUKI


Wanaume wenzangu tuelewe na pia hili lituingie akilini kwamba sisi na wake zetu tumeumbwa tofauti sana. Kila mwanamke ndani ya moyo wake na nafsi yake kuna kiu isiyo na msimu. Kiu iliayo kwa sauti ikitamani kudekezwa, kupendwa, kujaliwa na kuangaliwa kwa upendo kama mtoto mdogo. Sasa wewe leo mwenzako anadeka kidogo unamkurupusha kama mwizi eti "acha utoto weweee, unamdekea nani sasa" nani kakwambia mapenzi yana kukua, au yana ukubwa na udogo? Usiishi na mke wako kama mwanaume mwenzako, usimfanye yeye kama kifaa, yeye sio trekta au jiko au kompyuta au sufuria. Yeye ni kiumbe mwenye hisia tena kali tofauti kabisa na wewe. Kama haujafundishwa basi kamuulize mama yako atakwambia, na kama atakwambia tofauti basi mlaumu baba yako kwa kumfanya mama yako akawa kama wewe unavyomfanya mke wako leo. Pokea hiyo kwa leo - Chris Mauki

Kassim Mganga Feat. Christian Bella | Subira | Official Video

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...