Sunday 25 August 2013

Luteni Kanali wa JWTZ atoroka na nyaraka


Dar es Salaam. Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), linamtafuta ofisa wa jeshi hilo, Luteni Kanali, Colestine Seromba, baada ya kutoroka na kuelekea kusikojulikana.
Ofisa huyo aliyekuwa Mkufunzi katika Chuo cha Mafunzo ya Kijeshi cha Kompyuta kilichopo Dar es Salaam, anasadikiwa kutoroka na nyaraka muhimu za jeshi hilo tangu Desemba 18, mwaka jana.
Msemaji wa jeshi hilo, Meja Erick Komba akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya Jeshi jijini humo jana alisema, Seromba alikuwa na tuhuma za makosa ya kijeshi na ndiyo sababu ya kutoroka kwake.


“Wakati mchakato wa kumfungulia mashtaka ukiwa unaendelea ofisa huyo alitoroka usiku wa Desemba 17 kuamkia 18 mwaka jana, hivyo ofisa huyu ni mtoro kwa kipindi cha ziadi ya miezi minane,” alisema Meja Komba na kuongeza:
“Kijeshi kosa la utoro halifutiki, yaani halina ‘Time Bar’. Kwa maana hiyo bado ofisa huyu anaendelea kutafutwa na akipatikana hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.”Meja Komba alisema ofisa huyo ni Mtanzania mzaliwa wa Kijiji cha Rukira mkoani Kagera na si Mnywaranda kama ambavyo baadhi ya taarifa zinavyoenezwa.
Akijibu swali aliloulizwa kuhusu ofisa huyo kuwa Mkuu wa Chuo hicho, Meja Komba alisema alikuwa mkufunzi wa masomo ya kompyuta na taarifa nyingi alizokuwa nazo ni zile zilizowahusu wanafunzi yaani mahudhurio na matokeo yaliyowahusu wanafunzi.
“Mkuu wa chuo hicho hakuwa yeye alikuwa Kanali Obeid ambaye naye amestaafu miezi sita sasa, lakini jeshi lilipoanza uchunguzi dhidi yake alikabidhi vitendea kazi vyake vyote,” alisema Meja Komba.
CHANZO: Mwananchi

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...