Wednesday 28 August 2013

JESHI LA POLISI KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM LIMEWATIA MBARONI MAJAMBAZI TISA

 Jeshi la polisi kanda maalumu ya Dar es salaam limewatia mbaroni majambazi tisa wa kutumia siraha akiwemo askari polisi wa kituo cha Kipolisi oysterbay  jijin Dar es salaam.


Kamishna wa polisi kanda maalumu ya Dar es salaamu  Bw.suleimani Kova amesema majambazi hao wamekamatwa katika operesheni maalum ya jeshi hilo ambapo pia walifanikiwa kukamata sare za jeshi la wananchi Tanzania(JWTZ) zinazoaminika kutumika katika uhalifu pamoja na silaha na risasi
Aidha kamanda kova ameeleza kukamata magari yanayosadikika kutumika katika uhalifu tofauti pamoja na yenye namba za usajili T865CEH aina ya carina,na T967 AUG carina.
CHANZO: Habari za kitaifa-ITV

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...