Saturday 14 September 2013

BODA BODA ZINASAIDIA AU NI MAJANGA?

Usafiri wa pikipiki maarufu kama ``boda boda`` hutumika na wengi katika sehemu mbalimbali barani Afrika.Ni usafiri mzuri kama usalama ukizingatiwa. Tatizo tulionalo ni kuwa usafiri wa boda boda hauzingatii kabisa usalama wa abiria na dereva bila kusahau sheria za barabarani(sina uhakika maana wakipakiza mshikaki sijui kama wanakamatwa au la).Boda boda nyingi zimekuwa zikipakiza abiria zaidi ya mmoja,maarufu kama ``mshikaki`` bila kujali usalama wa waliopanda pikipiki hiyo.Unakuta boda boda imepakia watu watano na hakuna aliyevaa kofia ya kujilinda na ajali,au unakuta ni dereva tu ndiye amevaa kofia ya kujilinda na ajali.Hivi wadau, bodaboda ina uwezo wa kubeba watu wangapi?Je,boda boda ina uwezo wa kubeba watu zaidi ya bajaji?Mimi hapa sielewe na ndiyo maana kwangu naona boda boda ni JANGA kama hazitatumika kwa kuzingatia vigezo vya usalama barabarani.
Hebu angalia aina za mishikaki katika picha hapa chini.Kuna mshikaki wa watu watatu, wanne,watano n.k


Boda boda in Kenya


Boda boda in Kampala


Boda boda Kampala


Boda boda, Sudan








Familia katika boda boda ,Uganda!



No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...