Thursday 25 April 2013

NINI KIFANYIKE KUMKOMBOA MWANAMKE?




Kuni ambayo hutumika kama nishati ya kupikia hufuatwa mbali na kwa wengi wao hili ni zoezi la kudumu


Hawa wamebahatika kuwa na maji jirani
 
Ukamuaji wa maziwa ni moja ya kazi za wakina mama katika jamii nyingi

Wanawake  wengi hutembea umbali mrefu kupata mahitahi mbalimbali ya familia

Kutokuwepo uhakika wa maji hufanya wanawake wengi kufuata maji mbali
 
Baadhi ya wanawake wameelemewa na mzigo wa kazi za nyumbani zikiwemo kupika,usafi, kuchota maji na kutafuta kuni pamoja na kulima na kujitafutia kipato. Wanawake wenye wakati mgumu sana ni wale wa kijijini na ambao ndiyo wengi.
Kitakachoweza kumkomboa mwanamke ni ELIMU.

Faida ya elimu kwa wanawake ipo katika  nyanja zote katika jamii. Mbali na kuchangia kwenye uchumi wa taifa, wanawake wenye elimu ni muhimu katika  sekta binafsi kwani wengi wao huweza kujiajiri wenyewe na kuacha kuwa tegemezi kwa waume zao.
Elimu kwa wanawake pia kuhusishwa na ongezeko katika pato la familia,afya na lishe bora, uangalizi  mzuri wa watoto, n.k

Wanawake walioelimika huchelewa kuolewa na  huzaa watoto wachache.
 Kwa kila mwaka wa elimu kwa mwanamke hupunguza asilimia 7-9 ya vifo vya watoto.
Je,wanawake wanaweza kufanyanini ili kuboresha kipato?Tukutane katika muendelezo wa makala hii.

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...