Monday 15 July 2013

Tyson Gay na Asafa Powel walitumia madawa haramu

Asafa na Gay ni miongoni mwa wanriadha shupavu duniani


Wanariadha wawili kati ya wanariadha wenye kasi kubwa duniani -- Tyson Gay, kutoka Marekani na Asafa Powell wa Jamaica -- wamepatikana na kosa kutumia madawa ya kusisimua misuli.
Gay, ambaye ni mwanariadha wa pili kwa kuwa na kasi kubwa ya kukimbia katika mbio za mita mia moja, amesema anajiondoa kwenye mashindano ya dunia ya riadha yanayotarajiwa kufanyika mjini Moscow mwezi ujao.
Asafa Powell, ambaye alishikilia rekodi ya mbio za mita 100 hadi ilipovunjwa na Usain Bolt mwaka 2008, amekanusha kuwa alitumia dawa hizo makusudi.
Mwanariadha mwenzake wa Jamaica Sherone Simpson pia amepatikana na hatia ya kuzitumia dawa hizo za kusisimua misuli.
CHANZO: BBC

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...