Friday 23 August 2013

MWAKYEMBE ‘AWAWAKIA’VIGOGO WA BANDARI DAR



Dar es Salaam. Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe amewataka watendaji katika Bandari ya Dar es Salaam kuhakikisha wanajituma kwa uwezo wao na asiyeweza aende akakaange chipsi kwani itakuwa ndiyo kazi anayoweza.
Dk Mwakyembe aliyasema hayo jana katika mkutano wa wadau wa uchukuzi wa bandari kuhusu Matokeo Makubwa Sasa (BRN) kwa Bandari, mkutano uliofanyika Dar es Salaam.

“Tuna mpango wa kuboresha bandari kwenye nyanja mbalimbali kama vile kuongeza wafanyakazi wenye ujuzi na kuboresha mazingira ya bandari kwa ujumla ili kufikia mwaka 2015 bandari yetu iwe na uwezo wa kuingiza takriban tani 12.1 hadi tani 18 ya mizigo kwa mwaka” alisema na kuongeza:
Alisema wizara yake imejipanga kikamilifu kutekeleza majukumu iliyopewa na Serikali kuhakikisha wananchi wanayaona matokeo ambayo yatawanufaisha na kuinua uchumi wa nchi na kuwataka watendaji kufanya kazi kwa kujituma zaidi.
Dk Mwakyembe alisema Serikali inajipanga kuhakikisha Bandari ya Dar es Salaam inaboresha utendaji wake na kuwa miongoni mwa Bandari bora Afrika Mashariki ikiwa ni pamoja na kuondoa urasimu unaokwamisha utendaji wake.
Kwa muda mrefu, Dk Mwakyembe amekuwa akifuatilia kwa karibu utendaji wa watendaji wa Bandari ikiwemo kuwasimamisha viongozi saba, akiwemo Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari nchini (TPA), Ephraim Mgawe.
Dk Mwakyembe alisema baada ya kuusimamisha uongozi kuwa uamuzi wake umekuja baada ya kubainika kuwepo kwa matatizo yanayokwamisha ufanisi wa shughuli za mamlaka hiyo ikiwa ni pamoja na mgongano wa kimasilahi ambapo viongozi wa ndani ya mamlaka hiyo wamekuwa na kampuni zao zinazohudumia bandari.
CHANZO: Mwananchi

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...