Sunday 1 September 2013

MKOA KWA MKOA: TEMBELEA MKOA WA IRINGA KATIKA PICHA

Iringa ni mojawapo ya miji ya kihistoria nchini Iringa ilianzishwa mwaka 1892 kama kambi la jeshi la kikoloni wakati wa vita ya Wajerumani dhidi ya Wahehe. Wahehe waliongozwa na kiongozi wao,Chifu Mkwawa ambaye makao yake makuu yalikuwa KalengaAsili ya jina la Iringa ni neno la Kihehe "liliga" lenye maana ya boma. Mji umejengwa juu ya mlima ukitazama mto Ruaha bondeni.
Mji wa leo upo mahali pa "Neu Iringa" au Iringa mpya ya Wajerumani waliotumia jina hili baada ya kuharibu boma la mtemi Mkwawa huko Kalenga waliloita "Iringa" tar. 31 Oktoba 1894.
Mkoa wa Iringa una vivutio kadhaa vya utalii kama Isimila, jiwe la Gangilonga, makumbusho ya mkwawa huko Kalenga, mbuga za Ruaha n.k.Tuanze safari ya kuutembelea mji wa Iringa na vivutio vyake katika picha!

View of Iringa

iringa panorama


Picha juu zinaonyesha mwonekano tofauti wa mji wa Iringa

Central bus terminal
Stendi kuu ya mabasi-Iringa


Mapango ya Kitwiru ambapo Mkwawa na majeshi yake  walijificha na kupanga mashambulizi dhidi ya Wajerumani.Mapango haya yapo umbali wa kilomita 5 toka Iringa mjini.


Mnara wa majimaji ukiwa na majina ya wapiganaji waliofariki katika vita vya majimaji kati ya mwaka 1905-1907. Mnara huu upo Iringa mjini karibu na kituo kikuu cha Polisi.


Kifaa cha kivita cha Wajerumani kilichokamatwa na wapiganaji wa Kihehe wakiongozwa na Chifu Mkwawa wakati wa vita dhidi ya Wajerumani. Kifaa hiki kimeweka nje a ofisi za  Mkuu wa Wilaya ya Iringa kama alama ya ushindi mkubwa dhidi ya utawala wa kikoloni wa Wajerumani
River in Iringa
Mto Ruaha,Ipogolo




Soko kuu la Iringa lililojengwa kwa  kutumia usanifu wa Kijerumani likiwa limerembeshwa kwa miamba ambalo ni la kwanza kujengwa katika Afrika katika miaka ya  1930


Kanisa la Tosamaganga


Fuvu la Chifu Mkwawa lililopo katika makumbusho yake Kalenga



Makumbusho ya Chifu Mkwawa yaliyopo Kalenga


Isimila-sehemu iliyopatikana zana za mawe ambazo  zilitumiwa na binadamu wa mwanzo




Jiwe la Gangilonga


Iringa
Barabara ya Uhindini



Iringa mjini



870_ruaharivercamp_river.JPG


Tembo katika hifadhi za taifa za Ruaha


Ruaha River Lodge

1 comment:

  1. Used to teach physics at Mkwawa High School in the 1960s - Rod stanley

    ReplyDelete

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...