Thursday 19 September 2013

MKOA KWA MKOA: TEMBELEA MKOA WA KILIMANJARO KATIKA PICHA

Lengo na dhumuni la mkoa kwa mkoa ni kufanya watu waelewe vivutio mbalimbali vilivyomo katika mikoa yetu kwa kuona picha na maelezo mafupi.
Makao makuu ya mkoa wa Kilimanjaro ni Moshi.Mkoa huu umepakaa na nchi ya Kenya kaskazini mashariki, mkoa wa Tanga kusini  mkoa wa Manyara kusini magharibi na mkoa wa Arusha magharibi.Makabila makubwa mkoani humo ni Wachagga na Wapare ambapo pia kuna makabila mengine madogo madogo kama Wamasai na wakamba.
Mkoa wa Kilimanjaro una vivutio vikubwa vya utalii ikiwamo hifadhi ya taifa ya Kilimanjaro ambayo ndani yake kuna mlima Kilimanjaro


File:Entrance to Kilimanjaro National Park.JPG
Hili ni lango la kuingilia katika hifadhi za Taifa za Kilimanjaro 

Mlima Kilimanjaro
Kilimanjaro ni mlima mrefu kuliko yote Afrika. Una urefu wa mita5,895 (futi 19,340).Kilimanjaro ni kama safu ndogo ya milima mitatu: Kibo, Mawenzi na Shira.Kilimanjaro ni volkeno iliyolala kwa sasa. Kwenye kilele cha Kibo gesi bado inatoka. Kwa Kumbukumbu ya wenyeji  mlipuko wa mwisho ulitokea  mnamo mwaka 1730.
Kilele cha juu cha Kibo kinaitwa Uhuru. Mtu wa kwanza wa kufika kileleni hapo alikuwa Johannes Kinyala Lauwo kutoka Marangu aliyewaongoza Wajerumani Hans Meyer na Ludwig Purtscheller tarehe 6 Oktoba 1889 wakati wa ukoloni wa Ujerumani.
Kibo ina theluji na barafuto "mto wa barafu" kadhaa ndogo.

Picha:Kilimanjaro 2006-08-13.JPG
Mlima Kilimanjaro unavyoonekana kutoka Moshi

Picha:Kibo summit of Mt Kilimanjaro 001.JPG
Kilele cha Kibo kwenye mlima Kilimanjaro



Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro
Katika hifadhi hizi kuna wanyama wa aina mbalimbali kama nyani wa bluu, tembo, chui, nyati n.k
PICHA: Baadhi ya wanyama wapatikanao katika hifadhi za Kilimanjaro

  
  
 

Mji wa Moshi katika picha

Mji wa Moshi unasifika kwa usafi na utunzaji wa mazingira



Mitaa ya mji wa Moshi.Angalia jinsi mlima Kilimanjaro unavyoonekana

Ukiwa Moshi kuna hotels na lodges nyingi unaweza kupumzika na kupata chakula.Tuzione baadhi katika picha:
  Impala hotel

Kilimanjaro crane hotels & safaris
Zebra hotel
Keys hotel


No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...