Sunday 3 November 2013

NINI KIFANYIKE KUKOMESHA MAUAJI YA TEMBO?

TUGOME KUNUNUA BIDHAA ZOTE ZILIZOTENGENEZWA KWA MENO YA TEMBO.
Sambaza ujumbe huu !

Utajiri wetu kutokana na tembo hawa hatarini kuupoteza kama hatua zinazostahili hazitachukuliwa haraka


Pembe za ndovu

Tumekuwa tukisoma na kuangalia habari tofauti kuhusu tembo wanavyouwawa na pembe zao kuchukuliwa. Ujangili dhidi ya tembo umeshamiri licha ya kauli mbalimbali kutoka katika vyombo tofauti vya kitaifa na kimataifa za kusimamisha mauaji hayo zinazotolewa.
Tanzania inaoongoza kwa uuzaji nje wa pembe za ndovu.
Inakadiriwa kuwa wastani wa tembo 10,000 huuwawa kila mwaka nchini Tanzania.
Je, nini ni chanzo cha kuuwawa kwa tembo hao?
Huku tukipambana na jinsi ya kumaliza mauwaji ya tembo wetu,soko la pembe za ndovu limekuwa likishamiri huko Asia(China).Pembe za ndovu ambazo si halali zikifanikiwa kuingia nchini China basi hugeuka kuwa halali.
Kwa mtazamo wangu nadhani vitaa hii inabidi ipiganiwe pande zote yaani ni jinsi gani tutakomesha uwindaji huu haramu nchini mwetu na pili ni jinsi gani tutashughulika na wanunuzi wa pembe haramu.
Nadhani hapa ndipo penye changamoto zaidi kwani kunapokuwa na mwanya katika sheria ndipo watu hufanya yao.Kama wanunuzi wangebanwa na sheria za manunuzi ya pembe za ndovu sidhani kama ujangili huu ungekuwepo kwa kiasi hiki tunachoona sasa. Ni vizuri kukawa na sheria za kitaifa na kimataifa zisizokinzana katika kutekeleza hili. Kwa kufanya hivi tunasuru si tembo tu bali maliasili yote kwa ujumla.


Kukamatwa kwa vipande saizi ya 700 za pembe za ndovu inaonyesha jinsi gani uzao wa mnyama huyo asiye na hatia unavoelekea kumalizwa nchini.Inasikitisha na kutia hasira.Hivi tutavieleza nini vizazi vijavyo?
Tumeona wachina waliokamatwa na pembe za ndovu walivyojiamini na kuja kukusanya pembe nchini kwetu kama vile hakuna sheria.Wameonyesha jinsi gani walivyojihalalishia ukusanyaji wa nyara hizo.Watu wetu wakimatwa na madawa ya kulevya kwao wanawanyonga au kuwafunga kifungo cha muda mrefu,sisi tutawafanya nini hawa tuliowakamata?Sheria zetu zinasemaje?
NINI KIFANYIKE KUTOKOMEZA BIASHARA YA MENO YA TEMBO?
Hili ni swala la kuingizwa katika katiba mpya (kama halipo) kuwa atakayeshikwa na nyara za serikali ,au kujihusisha na uwindaji haramu ahukumiwe kama mhaini iwe ni raia au siyo na tusikubali kubadilishana wafungwa(extradiction) wa aina hii.
Sijui sheria yetu inasemaje kuhusu kukamatwa na nyara ila hawa Wachina inabidi wawe somo kwa wawindaji na wanunuzi haramu wengine wote kwani wamekutwa na kielelezo mikononi mwao.Kikubwa wautaje mtandao wao ili sheria ichukuwe mkondo wake.
Watanzania tuisaidie serikali yetu katika kutokomeza tatizo hili.Nina imani kuwa wapo wanaowajua watu wanaojishughulisha na biashara hii haramu.Tuwe na moyo wa uzalendo katika kulinda maliasili zetu.
Kingine "tugomee kununua bidhaa zote zilizotengenezwa kwa pembe za ndovu!Tukigoma kununua bidhaa mauwaji ya tembo yatakwisha.


Tembo katika hifadhi za Serengeti



Je,nini hutengenezwa kwa pembe za ndovu?
Pembe za ndovu hutumika  kutengeneza mapambo ya aina mbalimbali ya nyumbani na kwaajili ya urembo vilevile.Mfano wa mapambo hayo angalia picha zifuatazo:

  


Imeandikwa na Anna Nindi

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...