Kwa kweli huu ni zaidi ya unyama! Mimi nauita ni USHETANI ULIOPINDUKIA! Naomba kwa dhati kabisa mume huyu asiyekuwa na sifa za kuitwa mume afikishwe kwenye vyombo vya sheria kwani alichokifanya ni jaribio la mauaji yaani "attempted murder". Ashitakiwe na ikibidi afungwe jela ili iwe fundisho kwa wanaume wengine wanyanyasaji. Kama mwanaharakati naomba wana ukoo wa Mama Linda Mfinanga waungane pamoja na mashirika mbalimbali yanayopigania haki za kina mama nchini kuhakikisha kwamba haki inatendeka. Mama Vallery Msoka wa TAMWA, Dr Hellen Kijobisimba wa LHRC, na mashirika mengine lukuki chondechonde onyesheni uwepo wenu katika jambo hili. Naamini mama Linda ni mfano tu wa mamia kwa maelfu ya kinamama wanaopitia kwenye tanuru la mateso makuu katika familia zao.
Huu ni unyama wa aina yake na unastahili kupingwa kwa nguvu zote
ReplyDeleteKwa kweli huu ni zaidi ya unyama! Mimi nauita ni USHETANI ULIOPINDUKIA! Naomba kwa dhati kabisa mume huyu asiyekuwa na sifa za kuitwa mume afikishwe kwenye vyombo vya sheria kwani alichokifanya ni jaribio la mauaji yaani "attempted murder". Ashitakiwe na ikibidi afungwe jela ili iwe fundisho kwa wanaume wengine wanyanyasaji.
ReplyDeleteKama mwanaharakati naomba wana ukoo wa Mama Linda Mfinanga waungane pamoja na mashirika mbalimbali yanayopigania haki za kina mama nchini kuhakikisha kwamba haki inatendeka.
Mama Vallery Msoka wa TAMWA, Dr Hellen Kijobisimba wa LHRC, na mashirika mengine lukuki chondechonde onyesheni uwepo wenu katika jambo hili. Naamini mama Linda ni mfano tu wa mamia kwa maelfu ya kinamama wanaopitia kwenye tanuru la mateso makuu katika familia zao.