Tuesday 21 January 2014

SOMA ALICHOANDIKA DIAMOND PLATNUMZ KWENYE INSTAGRAM





diamondplatnumz:  Kama unakumbukumbu nzuri wakati nafanya tamasha langu la Christmass na Ngololo niliuliza mtoto atakae cheza vizuri Ngololo na kushinda nimpe zawadi gani?...na wengi walisema Nimuendeleze kielimu.... Hawa ndio washindi wetu walioshinda siku ile, ambao siku ya leo niliwapeleka Rasmi katika Shule ya East Africa International School iliyopo Mikocheni Dar es salaam ili waanze Masomo yao...Niliona ni vyema kama mtoto yupo shule ya kawaida nimuhamishe international school ili niweze kumsaidia elimu bora zaidi...Niushkuru pia uongozi Mzima na wanafunzi wa Shule ya East Africa International School kwa kuwapokea vizuri  
KWA PICHA ZAIDI BOFYA "READ MORE"


 Ni EAST AFRICA INTERNATIONAL
 SCHOOL,iliyopo mikocheni jiji Dar,kiukweli ni 

moja ya shule ambayo,mbali  na kuwa na
 mazingira mazuri ya kusomea,ni shule moja 
wapo zinazotoa elimu
 bora kabisa ,nina
 imani watoto hawa,wataitumia vizuri nafasi hii..kusoma 
kwa bidii ili kutimiza ndoto zao na siku moja wawe vijana wenye
 manufaa kwa taifa....

 Baadhi ya watoto wanaosoma shuleni hapo
 Jengo la utawala
CHANZO: Thisis diamond
ANGALIZO: Napenda kumpongeza Diamond kwa moyo wa kurudisha anachopata kwa jamii kwani kutoa ni moyo na si utajiri.Tunaona mfano wa wasanii wengi ambao hujisifia kutwa kwa kutaja kipato chao lakini hatujasikia nini wamerudisha kwa jamii kutokana na support ya kazi zao wanayoipata. Amefanya kitu kikubwa sana kwa kuwapa watoto "ELIMU BORA".
Wito kwa wazazi wa watoto hao wasibweteke,wasaidie katika kusimamia maendeleo ya watoto wao ili kuhakikisha kuwa wanafikia malengo yaliyokusudiwa.Big up Diamond Platnumz!
Na Anna Nindi

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...