Thursday 15 May 2014

DIAMOND PLATNUMZ ATAJWA KUWANIA TUZO ZA BET AWARDS 2014 MAREKANI

Baada ya kunyakua tuzo 7 za KTMA 2014, na kuwa nominated katika tuzo za MTV ‘MAMA’ nchini Afrika Kusini, sasa Diamond Platnumz ametajwa kuwania tuzo kubwa zaidi za kimataifa BET Awards za nchini Marekani.
Diamond (2)
Hit single yake ya ‘Number 1’ ndio iliyompa tiketi Diamond kuwa nominated katika kipengele cha ‘Best International Act: Africa’, ambapo anachuana na mastaa wengine wa Africa ambao ni Davido(Nigeria), Mafikizolo (Afrika Kusini), Sarkodie (Ghana), na Tiwa Savage (Nigeria).



Diamond ndiye msanii pekee wa Afrika mashariki katika tuzo hizo.
Hivi ndivyo ilivyoandikwa katika mtandao wa www.bet.com
BEST INTERNATIONAL ACT: AFRICA “NUMBER ONE” (TANZANIA)
TANZANIAN STAR DIAMOND PLATNUMZ BECAME A GLOBAL FORCE WITH SUCCESS OF HIS HIT “NUMBER ONE” AND THAT WAVE MAY CONTINUE WITH A WIN FOR BEST INTERNATIONAL ACT: AFRICA.

bet
Sherehe za ugawaji wa tuzo hizo zitafanyika June 29 huko Los Angeles, Marekani
Tuzo za BET huandaliwa na kituo cha TV cha Black Entertainment Television, na zilianzishwa mwaka 2001 kusheherekea mafanikio ya kazi za Wamarekani weusi katika sanaa ya muziki, uigizaji, michezo na maeneo mengine ya burudani.
Hongera sana Diamond Platnumz, endelea kuipeperusha vizuri bendera ya Tanzania.
CHANZO: Bongo5

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...