Msanii wa
Bongo Movie, Rachel Haule 'Recho' (pichani), amefariki dunia usiku wa kuamkia
leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es slaaam. Habari
zilizotua Global na kuthibitishwa na Mwenyekiti wa Bongo Movie, Steve Nyerere,
zimesema kuwa Recho alikwenda Muhimbili jana kujifungua ambapo mara baada ya
kujifungua mtoto alifariki na yeye hali yake kuwa mbaya, ilibidi ahamishiwe ICU
ambako hali ilizidi kuwa mbaya na baadae kufariki dunia.
Kifo cha
Recho kimekuja ndani ya wiki moja baada ya kufariki kwa msanii mwingine wa
Bongo Movi Adam Kuambiana Jumamosi iliyopita, kifo hiki kimeleta mstuko mkubwa
kwenye tasnia ya ya filamu za kibongo. Habari na picha zaidi zitawajia baadae.
No comments:
Post a Comment