Thursday 15 May 2014

MVUA NOMA: MAFURIKO TANGA








Nyumba zisizopungua 80 zimezingirwa na maji yaliyotuama kupelekea ya mvua kali zinazoendelea jijini Tanga 

Wito unatolewa kwa viongozi wa serikali za mitaa kusimamia zoezi la uzibuaji wa mifereji (mitaro) iliyoziba ambayo imepeleka maji kutuama na kuzingira makazi ya watu.

Vile vile kuna mitaa ambayo ujenzi umesongamana hali hiyo imesababisha maji kukosa njia ya kupita kuelekea maeneo yenye michirizi hivyo ni vyema kutathmini njia za mbadala za ujenzi.

Jukumu la usafi wa mazingira ni la kila mwananchi katika maeneo wanayoishi hivyo ni vyema juhudi zikafanyika kwa kila eneo kuzibua mifereji na kuchimba mifereji ili kusaidia maji kupita na kuto tuama 

Kufuata ushauri huu kutasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza au kuepuka mafuriko na kuepusha magonjwa ambukizi.

Maeneo yaliyo katika hali ya kuzingirwa na maji ni pamoja na Usagara, Magaoni,Magomeni, Kwanjeka, Sahare na mengineyo.



CHANZO: Tanga na matukio

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...