Thursday 28 May 2015

THE KITCHEN: JINSI YA KU-DESIGN JIKO NA UPANGILIAJI WAKE


Mandhari nzuri ya nyumba huchangiwa na vitu vingi ikiwamo na mpangilio mzuri wa jiko. Jiko hutakiwa kujengwa kukidhi mahitaji yote ya jikoni. Kila kitu hutakiwa kuwa mahali pake,kuanzia vyombo hadi mashine ndogo za jikoni.Unaweza ukawa umejengewa jiko vizuri sana ila wewe mwenyewe usiwe na uwezo wa kupanga vitu vyako vizuri ukaweka sufuria hapa,sahani pale,blender hapa,matunda yametapakaa tu kwenye meza za jikoni, vyombo vichafu vimejaa tele katika sinki, ili mradi mtu akiingia anaona kama vile yupo stoo badala ya jikoni.Jikoni kunatakiwa kuwe safi muda wowote na ikibidi mtu akiingia asijue kabisa mmekula nini!Maana kuna majiko ukiingia unajua kabisa hawa leo wamekula samaki n.k! Unaweza usisikie harufu bali kukawa na mabaki labda katika sinki au vyote kwa pamoja ( yaani mabaki na harufu).

Angalia picha zifuatazo utaona jinsi jiko linavyotakiwa kuonekana muda wote.Kazi kwako! 













No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...