Wakazi
wa kitongoji duni cha Mathare katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, sasa
wanaweza kupata maji safi ya kunywa na kwa matumizi mengine.
Mpango
unaoungwa mkono na serikali umezinduliwa kwenye mji mkuu wa Kenya
Nairobi unaowawezesha watu wanaoishi kwenye mitaa ya mabanda kununua
maji kwa kutumia kadi.
Vituo vya kuuza maji vimebuniwa kote katika
sehemu za mabanda ambapo wenyeji hutumia kadi zilizo na pesa kununua
maji safi na kwa bei nafuu.
Wenyeji wa mitaa ya mabanda
nchini Kenya wamekuwa na tatizo la kupata maji safi ambapo hulazimika
kununua maji kwa bei ghali kutoka kwa wauzaji au kutoka kwa magenge
ambayo hudhibiti na kuuza maji hayo kwa kuyachuuza.
Mradi kama huo
umefaulu katika baadhi ya maeneo ya vijijini nchini Kenya, lakini hii
ni mara ya kwanza kuzinduliwa katika mji huo mkuu.
Vituo hivyo vya kutoa huduma
hiyo ya maji vimefanikiwa kutokana na ushirikiano kati ya serikali ya
mitaa nchini Kenya na kampuni ya maji ya Grundfos ya Denmark.
Kampuni
ya kusimamia huduma ya usambazaji maji, ina mikakati ya kuhakikisha
kuwa huduma hii walioianzisha itasambazwa kote katika mji mkuu wa
Nairobi na kwengineko nchini humo.
Huku hilo likianzishwa wakaazi wa mitaa kadhaa mjini Nairobi bado wanalalamikia ukosefu wa maji.
CHANZO: BBC SWAHILI
No comments:
Post a Comment