Monday 14 September 2015

TUSAIDIE WATOTO HAWA: COLLEGINE SISTERS OF HOLY FAMILY ORPHANAGE

Nilipokuwa jijini Tanga hivi karibuni nilibahatika kutembelea kituo cha watoto kijulikanacho kama COLLEGINE SISTERS OF HOLY FAMILY ORPHANAGE (Nyumba ya furaha).Kituo hiki kipo karibu na ilipokuwa Plaza Inn.Katika safari hii ambayo ilikuwa ni ya kifamilia tuliambatana mimi na ndugu zangu.
Kabla ya kwenda kituoni hapo,tuliwasiliana na masista walezi wa kituo hicho ili kujua mahitaji halisi kwa watoto hao kwani tulidhani ni vizuri kufanya hivyo kuliko kupeleka tu vitu hata visivyo na ulazima.
Hii tulifanya vizuri sana kwani tuliweza kugundua kuwa kuna watoto wachanga kabisa ambao walikuwa na mahitaji zaidi.
Siku moja kabla ya kwenda kituoni hapo tulinunua mahitaji kama walivyotaka.Siku hii kulikuwa na mvua kubwa ila haikutuzuia kufanya manunuzi. Tulinunua maziwa, lactogen 1 & 2, pampers na juice. Hivi ndiyo vitu walivyotaka tuwapelekee.

Mtoto mdogo kuliko wote, Sophia, miezi mitano (5).Aliokotwa akiwa na siku 3 baada ya kuzaliwa
Mtoto George mwenye umri wa miezi 7

Bonyeza READ MORE kusoma habari yote na kuona picha zaidi


Tulikwenda kituoni hapo siku ya jumamosi tukiwa watu watano (5).Kati ya hawa watu mmoja alikuwa ni mtoto wa miaka 14. Huyu ni mtoto wa kaka yangu.Tulimchukua kama njia ya kumfanya anapokua ajue kuwa jukumu la kusaidia wenye mahitaji ni la jamii yote akiwemo yeye.
Kituoni hapo tulipokelewa vizuri na masista pamoja na watoto.Sista aliyekuwa na sisi katika tukio hilo ni sista Marcelina.Sista Marcelina alitueleza historia ya kituo kwa ufupi.
Kituo kilianzishwa mwaka 2006 kikiwa na watoto 14 tu. Kwasasa kituo kina watoto 54 wa umri tofauti. Mtoto mdogo kabisa, Sophia, ana miezi mitano(5).Na mwingine, Georgr, ana miezi saba (7).
Watoto wa kituoni hapo wanasoma shule mbali mbali zilizopo Tanga mjini na sehemu nyingine. Kuna watoto ambao wamemaliza sekondari na wanafanyakazi na kuna wengine wapo vyuoni.
Katika kusaidiana ulezi, watoto wenye umri mkubwa husaidia kuwaangalia wadogo zao.Kwa kweli ni hali ambayo inagusa sana kwa uhalisia.Kikubwa na chenye kutia faraja, watoto wote wana furaha sana.Walifuahi sana kutuona na tukaongea pamoja na kucheza nao huku wakapiga picha nyingi na sisi.

Kituo kilianzia katika nyumba hii

Kituo hiki kilianza na nyumba ndogo ya kawaida ya kuishi na kwa jinsi siku zilivyokwenda na idadi ya watoto kuongezeka nyumba ilikuwa ndogo hivyo kupelekea kuanza kujenga jengo lingine la ghorofa 2 pembeni.Ujenzi wa jengo hilo unaendelea bado na unafanikishwa kutokana na michango ya wadau mbalimbali.

Jengo jipya la kituo

Ningependa kutoa wito na kuwaomba wale wote wenye mapenzi mema wawasaidie watoto hawa kwani kutoa ni moyo na si utajiri. Kumbuka kila kidogo utakachopeleka kitabadilisha maisha ya watoto hawa na Mungu atajaza pale ulipopunguza. Badala ya kutumia pesa kwa kunywa pombe au kuhonga ni bora ukawasaidia watoto hawa upate Baraka za Mungu.
Watoto bado wana mahitaji mengi ikiwemo chakula, nguo n.k.Vilevile jingo lao linahitaji kukamilika.

Nitaweka namba ya sister Marcelina hapa kwa wale wanaotaka kusaidia watoto hawa. 






Watoto wakubwa wanasaidia kulea wadogo zao


Watoto wakiwa na nyuso za furaha

Watoto wakiwa kituoni
Jengo jipya la kituo

Lactogen 1 & 2 tulizopeleka

Juice tulizopeleka

Tukiwa na sister Marcelina na watoto

Sister Marcelina kulia akiwa na watoto pamoja na ujumbe wetu

Tukiwa na watoto

Mtoto huyu aliyepakatwa na kaka yangu, alimng´ang´ania hakukubali 
aliporudishwa kwa sister

Mtoto George, mwenye umri wa miezi 7, akiwa amelala baada 
ya kubembelezwa

Tukisaini ofisini


Mtoto wa miaka 14, Kelvin,ambaye tulifatana nae, 
akifurahi na mtoto

Tukiwa na baadhi ya watoto na sister Marcelina

Tulifarijika sana na safari hii. Asante nyingi kwa sister Marcelina na wahudumu wote wa kituo hiki.
MNAWEZA KUWASILIANA NA SISTER MARCELINA KWA NAMBA: 0765 565 007

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...