Friday 16 October 2015

UNAJISIKIAJE UKIWA CHANZO CHA KUVUNJA NDOA?

Kuna hili tatizo la ndugu wa mume kuingilia ndoa ya ndugu yao.Hii inahusu sana mawifi ambao wengi wao huwa ndiyo chanzo cha ndoa nyingi kuvunjika.Na wengi hufanya hivi kwa maslahi yao binafsi na wala si kwa maslahi ya kaka zao. Ukichunguza wengi ya mawifi hawa ni umaskini na roho mbaya tu ndiyo huwa vinawasumbua. Ili watimize uovu wao hutafuta visingizio na hadithi nyingi za kutunga kuonyesha uovu wa  wifi wasiyemtaka wanaweza kusingizia kuwa wifi yao ni mshirikina n.k. Hakuna kitu kibaya duniani kama kusingizia mtu mambo yasiyokuwa  kweli kwani malipo yake huja vibaya. Vitabu vya dini vinakataza kumsingizia jirani yako uwongo, hivyo muwe makini kwani uwongo huenda ukawaponza.


Hapohapo wengine humtafutia kaka yao mwanamke ambaye wao wanatumaini kuwa watakuwa na manufaa nae. Ila huwa hawajui kuwa wanaweza kupoteza  kipande cha almasi na kuokota kipande cha chupa! Kuna kitabu cha hadithi kilichoandikwa na Hammie Rajabu kiitwacho “Gubu la Wifi”.
Katika kitabu hiki mawifi wawili walimchukia wifi yao bila sababu yeyote. Wifi yao aliwapenda sana na aliwafanyia mengi mema.Wao hawakujali hayo bali walikuwa wana mwanamke waliyempenda wao ambaye ndiye walitaka awe wifi yao. Walimfanyia  wifi yao vitimbi vyote na kuanza kumpika kaka yao kwa uwongo mpaka nae akaiva. Mwishoni akamwacha mkewe.
Akaolewa waliemtaka. Unajua nini kilitokea?Walilotegemea siyo lililotokea.Wifi mpya hakutaka kuwaona kabisa nyumbani kwake.Ni yeye ndiye aliwanyanyasa  mpaka wakamkumbuka wifi yao wa kwanza ambae alikuwa na upendo sana nao. Wifi wa kwanza akaolewa tena na mume mwenye nafasi yake nzuri kimaisha zaidi ya mume wa kwanza.
Jamani mawifi acheni roho mbaya.Kama mmeshindwa na maisha yenu msiharibu maisha ya watu wengine.Mungu hapendi sababu kusononeka kwa mke aliyeachwa kutawafanya nyie maisha yenu yapoteze mwelekeo kabisa.

MWENYE MASIKIO NA ASIKIE!

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...