Thursday 15 October 2015

USINYANYASWE NDUGU FANYA HAYA UWAPO MIKONONI MWA POLISI






Wengi hatujui haki zote na hii hupelekewa mtu kuonewa bila sababu. Soma hapa ujue haki zako uwapo mikononi kwa polisi.













( 1 )Askari  akikuweka   chini ya ulinzi  muulize  kitambulisho  ni  haki yako.

( 2 )Askari akikukamata akuoneshe  kitambulisho chenye muhuri wa mahakama  kama anasema ametumwa na mahakama kukumata, ni haki yako.

( 3 )Askari akikukamata akwambie kwanini anakukamata  na anakupeleka kituo gani, ni haki yako.

( 4 )Unaruhusiwa  na sheria kukataa kukamatwa hata kutumia nguvu kama hukuambiwa  sababu  ya  kukamatwa.

( 5 ) Askari anapokiuka taratibu za ukamataji anageuka na kuwa  mhalifu  ni haki  yako kujikinga naye.

( 6 )Askari haruhusiwi  kukuvuta shati, kukukaba koo, kukushika suruali kama hujakataa kutii amri  halali.


( 7 )Askari haruhusiwi kuondoka  na mtu mwingine baada ya kumkosa mtuhumiwa  halisi.

( 8 ) Askari  haruhusiwi  kupekua nyumba ya mtu bila kibali  cha kupekua.
( 9 )Askari lazima akuoneshe kibali cha kupekua na ukisome.

( 10 )Kibali kieleze jina la aliyekitoa, kituo kilipotolewa,jina la mtu au sehemu ya upekuzi, au uchanganuzi wa mtu au sehemu.

( 11 )Hairuhusiwi  kupekuliwa usiku kuanzia saa 1 jioni mpaka saa 12 asubuhi.

( 12 )Ni  haki yako kumpekua askari kabla  hajakupekua ili asipandikize kitu.

( 13 )Usipekuliwa nyumbani bila kuwapo kiongozi  wa mtaa.

( 14 )Kila kitakachochukuliwa katika upekuzi lazima kiandikwe na askari aweke sahihi.

( 15 ) Mali iliyochukuliwa  katika upekuzi lazima ibaki salama.

( 16 )Mwanaume haruhisiwi kumpekua mwanamke na mwamke haruhisiwi kwa mwanaume.

( 17 )Unaruhusiwa  kukataa kupekuliwa iwapo taratibu hizi hazikufuatwa.
( 18 )Askari haruhusiwi kukutukana wala kukupiga.

( 19 ) Unaruhusiwa kutozungumza lolote mpaka unayemuamini afike uwapo chini ya ulinzi, ni haki yako.

( 20 )Usilazimishwe kuongea au kuandika ambacho hutaki, ni haki yako.

( 21 )Usitoe maelezo bila uhakika yatatumika mahakamani yatakuletea shida.

( 22 )Unaruhusiwa kukaa kimya na usizungumze kitu  uwapo chini ya ulinzi.


HIZI ZOTE NI  HAKI  ZAKO, ZILAZIMISHE    USIBEMBELEZE WALA USIZIOMBE
CREDIT: sheriayakub bliog

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...