Wanaume wenzangu
tuelewe na pia hili lituingie akilini kwamba sisi na wake zetu tumeumbwa
tofauti sana. Kila mwanamke ndani ya moyo wake na nafsi yake kuna kiu isiyo na
msimu. Kiu iliayo kwa sauti ikitamani kudekezwa, kupendwa, kujaliwa na
kuangaliwa kwa upendo kama mtoto mdogo. Sasa wewe leo mwenzako anadeka kidogo
unamkurupusha kama mwizi eti "acha utoto weweee, unamdekea nani sasa"
nani kakwambia mapenzi yana kukua, au yana ukubwa na udogo? Usiishi na mke wako
kama mwanaume mwenzako, usimfanye yeye kama kifaa, yeye sio trekta au jiko au
kompyuta au sufuria. Yeye ni kiumbe mwenye hisia tena kali tofauti kabisa na
wewe. Kama haujafundishwa basi kamuulize mama yako atakwambia, na kama
atakwambia tofauti basi mlaumu baba yako kwa kumfanya mama yako akawa kama wewe
unavyomfanya mke wako leo. Pokea hiyo kwa leo - Chris Mauki
No comments:
Post a Comment