Kwenye Exclusive interview na millardayo.com Madee amehadithia kila kitu kilichomtokea wakati anaingia tu Afrika Kusini siku kadhaa zilizopita ambapo hii imetokea kutokana na ukubwa wa habari, uzito wa tukio la wale Watanzania wawili wasichana waliokamatwa kwenye kiwanja cha ndege Johannesburg wakiwa na dawa za kulevya wakitokea Tanzania.
Wednesday 31 July 2013
MKOA KWA MKOA: LEO TUPO SONGEA MKOANI RUVUMA
Unapozungumzia historia ya Tanzania basi hutaacha kuitaja Songea,ambayo ni makao makuu ya mkoa wa Ruvuma. Songea ndiyo ilikuwa makao makuu ya vita vya majimaji vilivopiganwa kati ya mwaka 1905-1907. Jina la Songea linatokana na kionozi wa Wangoni aliejulikana kwa jina la Songea Mbano. Songea pamoja na viongozi wengine wa Wangoni,walinyongwa na Wajerumani mwaka 1906.
Mbali ya kuwa mkoa wa Ruvuma ni maarufu kwa kilimo hususan mahindi,vilevile kuna utajiri wa mawe a vito aina ya sapphire na ruby.Kwa kumbukumbu zangu binafsi uchimbaji huu umeshamiri katika wilaya ya Tunduru.
Hii ni barabara ya kuelekea Songea
Mbali ya kuwa mkoa wa Ruvuma ni maarufu kwa kilimo hususan mahindi,vilevile kuna utajiri wa mawe a vito aina ya sapphire na ruby.Kwa kumbukumbu zangu binafsi uchimbaji huu umeshamiri katika wilaya ya Tunduru.
Hii ni barabara ya kuelekea Songea
Kanisa la Katoliki,Peramiho |
MWAKYEMBE AVUTIA PUMZI `UNGA` AIRPORT
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe |
Kufuatia matukio mfululizo ya kukamatwa kwa watuhumiwa wa dawa za kulevya wanaodaiwa kuwa ni Watanzania kwenye viwanja vya ndege nje ya nchi wakipitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema atalishughulikia suala hilo kama alivyofanya bandarini.
Dk. Mwakyembe ambaye wizara yake ndiyo yenye dhamana na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA), alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam wakati wa mazungumzo maalumu na NIPASHE kuhusu ufuatiliaji wa vitendo hivyo vinavyoharibu taswira ya nchi kimataifa.
`MEMORY CARD`YALETA HOFU WAKAZI BUTIAMA
Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Angelina Mabula |
Aina mpya ya ukatili wa kijinsia maarufu kama `memory card' unaohusisha wanawake kuuawa na kunyofolewa sehemu za siri, imezua hofu miongoni mwa wakazi wa wilaya Butiama mkoani Mara.
Kati ya kipindi cha Desemba mwaka jana na Julai, mwaka huu, jumla ya wanawake 14 wanasadikiwa kufanyiwa ukatili huo.
Ukatili huo umebainishwa na wanawake mbalimbali walipokuwa wakizungumza kwenye mdahalo wa kupinga ukatili wa wanawake na watoto wa kike uliofanyika katika kijiji cha Bisumwa, Wilaya ya Butiama mkoani Mara ambapo walisema mauaji hayo yanaongozwa na kundi la watu wanaojiita makhirikhiri.
SERIKALI YAWAACHIA WANANCHI KUHUSU MAFUTA YA UBUYU
Dar es Salaam. Serikali imesema suala la matumizi ya mafuta ya ubuyu sasa inawaachiwa wananchi wenyewe kutumia ama kuacha.
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, alisema hayo jana alipotoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari baada ya kufungua mkutano wa mafunzo ya wataalamu kutoka vitengo vya mbalimbali vya Udhibiti Dawa na Chakula visivyofaa kwa matumizi ya binadamu kutoka nchi 16 za Kusini mwa Jangwa la Sahara.
KESI YA LADY JAYDEE YAPIGWA KALENDA
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, leo imeiaharisha kesi inayomkabili msanii wa kizazi kipya nchini, Judith Wambura 'Lady Jaydee' a.k.a Annaconda dhidi ya uongozi wa Clouds Media Group hadi Agosti 2, mwaka huu.
Kesi hiyo ya madai iliyopo mbele ya Hakimu Athumani Nyamlani, leo ililetwa kwa ajili ya kusikilizwa lakini ilishindikana kutokana na wakili anayemtetea, Jaydee kutotokea mahakamani hapo na kumtuma mwakilishi wake.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa wakili huyo wa Jaydee, amekwenda katika Mahakama Kuu kuhudhuria kesi nyingine na hivyo kushindwa kufika mahakamani hapo kuendelea na kesi hiyo na hivyo kuahirishwa hadi Agosti 2, mwaka huu.
MBONI AANGUA KILIO MBELE YA MZEE RUKSA
Na Mwandishi Wetu
HOSTI wa Kipindi cha ‘The Mboni Show‘ kinachorushwa kupitia Kituo cha Runinga cha EATV, Mboni Masimba Jumapili iliyopita aliangua kilio mbele ya Rais Mstaafu wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi walipokuwa kwenye hafla ya kufuturisha kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
HOSTI wa Kipindi cha ‘The Mboni Show‘ kinachorushwa kupitia Kituo cha Runinga cha EATV, Mboni Masimba Jumapili iliyopita aliangua kilio mbele ya Rais Mstaafu wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi walipokuwa kwenye hafla ya kufuturisha kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Mtangazaji huyo alimwaga machozi wakati akiwakaribisha wageni waalikwa pamoja na kutoa shukrani zake kwa wote waliomsaidia kufanikisha shughuli hiyo.
Baada ya kutoa shukrani alionekana kuwa mwenye furaha kwa kumtambulisha baba yake mzazi, mzee Masimba ambaye hajulikani kwa watu kama ilivyo kwa mama yake.
Baada ya kutoa shukrani alionekana kuwa mwenye furaha kwa kumtambulisha baba yake mzazi, mzee Masimba ambaye hajulikani kwa watu kama ilivyo kwa mama yake.
MAPENZI YAUA
Hamida Hassan na Haruni Sanchawa
WAKATI Waislamu wakiwa ndani ya Mfungo wa Ramadhani, mapenzi yamemuua kijana Ibrahim Ibrahim ‘Ibra’ wa Kundi la Wakali Danta la Magomeni jijini Dar kwa kuchomwa visu.
WAKATI Waislamu wakiwa ndani ya Mfungo wa Ramadhani, mapenzi yamemuua kijana Ibrahim Ibrahim ‘Ibra’ wa Kundi la Wakali Danta la Magomeni jijini Dar kwa kuchomwa visu.
Waombolezaji wakiwa wamebeba mwili wa marehemu Ibra.
Tukio hilo la kusikitisha limetokea Julai 27, mwaka huu maeneo ya Magomeni Kagera ambapo ndugu wa Ibra, Ally Jumanne Sanane alidai kuwa, Ibra alichomwa kisu na kijana aliyefahamika kwa jina la Kelvin wakimgombea demu aitwaye Fatma Kiduku.
Mtoa habari huyo alidai: “Fatuma alikuwa ni mchumba wa Ibra lakini pia inaonekana alikuwa akitoka na Kelvin.
Mtoa habari huyo alidai: “Fatuma alikuwa ni mchumba wa Ibra lakini pia inaonekana alikuwa akitoka na Kelvin.
Tuesday 30 July 2013
Askari kituo cha Osterbay wakamatwa na meno ya tembo 70
WATU tisa, wawili kati yao wakiwa ni askari wa Jeshi la Polisi kituo cha Osterbay jijini Dar esalaam wamekamatwa wilayani Kisarawe Mkoani Pwani kwa tuhuma za kukutwa wakisafirisha meno ya tembo (ndovu) 70 sawa na kilo 305 kinyume na sheria. Meno hayo ya tembo kwa mahesabu ya kawaida ni sawa na Tembo 35 ndiyo wameuawa na kwamba thamani ya meno hayo ni zaidi ya sh, milioni 850 fedha za kitanzania.
IRENE UWOYA KUTOKA KIVINGINE NA SHOW YAKE YA KUTENGENEZA NA KUKARABATI NYUMBA ITAKAYO RUSHWA CLOUDS TV
Irene Uwoya anakuja na kipindi chake kipya cha Tv kwa ajili ya kutengeneza na kukarabati nyumba mbalimbali za watu atakazotembelea. Kipindi hicho kitarushwa kupitia Clouds Tv na tayari actress huyo ameanza kushoot kipindi hicho kama anavyoonekana pichani hapo juu. Irene Uwoya ni muigizaji mwingine aliyeamua kugeukia vipindi vya Tv pia ukiachilia mbali kuigiza filamu wengine ni Rose Ndauka na Wema Sepetu ambaye show yake kuhusu maisha yake halisi pia kitarushwa Clouds Tv kuanzia mwishoni mwa mwezi wa nane mwaka huu.
WAZIRI MKUU WA THAILAND YINGLUCK SHINAWATRA AWASILI NCHINI KWA ZIARA RASMI YA SIKU TATU
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimlaki Waziri Mkuu wa Thailand Mhe Yingluck Shinawatra alipowasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Julai 30, 2013 kwa ziara rasmi ya siku tatu nchini.
Akisalimiana viongozi wa Tanzania....
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimlaki Waziri Mkuu wa Thailand Mhe Yingluck Shinawatra alipowasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Julai 30, 2013 kwa ziara rasmi ya siku tatu nchini.
Waziri Mkuu wa Thailand Mhe Yingluck Shinawatra akikagua gwaride maalum la heshima lililoandaliwa kwaajili yake mara baada ya kuwasili nchini.
PICHA zaidi bofa READ MORE
MAMA SALMA KIKWETE KATIKA MKUTANO WA HIGH LEVEL GROUP-GABERONE -BOTSWANA
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama Salma Kikwete akipokea ua mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Sir Seretse Khama jijini Gaberone nchini Botswana kutoka kwa binti Jessica Kissasi, anayesoma darasa la pili, Baobab International School t arehe 29.7.2013.PICHA NA JOHN LUKUWI.Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokewa na Bwana Christopher Castle,Mkuu wa Idara ya HIV and Health Education kutoka Makao Makuu ya Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) yaliyoko Paris nchini Ufaransa wakati Mama Salma alipowasiri kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Sir Seretse Khama huko Botswana tarehe 29.7.2013.Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipewa maelezo mafupi na Dr. Patricia Machawira, Mshauri Mkuu wa HIV and AIDS wa Nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika muda mfipi kabla ya kuanza kwa mkutano wa “High Level Group-Action on comprehensive sexuality education and health services for adolescents and young people in Eastern and Southern Africa “ unaofanyika Gaberone nchini Botswana tarehe 30-31.7.2013.Baadhi ya wajumbe wa mkutano wa High Level Group wakisikiliza hotuba ya ufunguzi iliyokuwa ikitolewa na Mama Salma Kikwete .
Picha zaidi bofa READ MORE
PICHA ZIKIONYESHA MANDHARI MBALIMBALI YA MJI WA TANGA.WALE WA TANGA MPO?
Maeneo ya Chumbageni
Maeneo ya Chumbageni
Bandari ya Tanga inavyoonekana kwa mbali
AHUKUMIWA MIAKA 30 KWA KUMBAKA NA KUMZALISHA MWANAYE
Yusufu Amani (39) aliyembaka mwanaye wa kumzaa kisha kumzalisha baada ya kutengana na mkewe akiwa kizimbani.
Yusufu akificha sura yake asipigwe picha baada ya hukumu ya miaka 30.Kulia ni mtoto aliyebakwa na baba yake kisha kuzalishwa akiwa na mtoto wake wakati wakitoka mahakamani. Kushoto ni mama mzazi wa binti aliyebakwa na kuzalishwa.
Yusufu akificha sura yake asipigwe picha baada ya hukumu ya miaka 30.Kulia ni mtoto aliyebakwa na baba yake kisha kuzalishwa akiwa na mtoto wake wakati wakitoka mahakamani. Kushoto ni mama mzazi wa binti aliyebakwa na kuzalishwa.
MAHAKAMA ya wilaya ya Mbeya imemhukumu kwenda jela miaka 30 mkazi wa Isanga Mkoani hapa baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumlawiti na kumzalisha binti yake wa kumzaa akiwa na miaka 15( jina linahifadhiwa).
Mwendesha mashitaka wa serikali Archiles Mulisa aliiambia mahakamani hiyo Mbele ya Hakimu Gilbert Ndeuruo kuwa Mshtakiwa huyo ni Yusufu Amani (39) anayedaiwa kumbaka mwanaye wa kumzaa kisha kumzalisha baada ya kutengana na mkewe.
MARIO BALOTELLI-MCHEZAJI ASIYEISHIWA VITUKO.PICHA ZINAJIELEZA HAPA!
Mario Balotelli,mbali ya kuwa mwanasoka mzuri uwanjani,ni mchezaji anayeongoza kwa kuwa na vituko vingi. Je,unajua kuwa Mario ana mtoto?Fuatilia picha zake hapa kwani picha zenyewe zinaongea. |
Pia, mtoto wa Mario Balotelli akiwa na mama yake aitwae Raffaella Fico |
BILIONEA ALIYEMWAGIWA TINDIKALI DAR… HALI TETE
Na Mwandishi Wetu
HALI ni tete kuhusiana na tukio la bilionea Said Mohamed Saad kumwagiwa tindikali, athari ni kubwa. Jinsi alivyoharibika inatia simanzi lakini kumpata mhusika wa unyama huo ni kitendawili kinacholitega Jeshi la Polisi Tanzania.
Said ambaye ndiye mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Centre, yenye maduka mengi makubwa ya vitu vya nyumbani ndani ya Dar es Salaam na mikoa kadhaa ya Tanzania, anaendelea na matibabu nchini Afrika Kusini lakini mmoja wa watu waliomshuhudia, amefafanua jinsi hali ilivyo mbaya.
Subscribe to:
Posts (Atom)
PALM TREES ARE BEAUTIFUL
Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...
-
Dar es Salaam: Mwekezaji Sheikh Salim Abdullah ametangaza kuwekeza kwenye Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere Dar es Salaam (JN...