Monday 23 September 2013

NDUGU WA KENYATTA AUAWA, WATOTO WAKE WANUSURIKA

Hawa ni baadhi ya majeruhi wakipatiwa huduma ya 
kwanza na wasamaria wema , Picha na AFP    
          
Nairobi. Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ni miongoni mwa watu waliopoteza ndugu zao wa karibu katika tukio la mauaji ya kigaidi lililotokea Jumamosi katika duka kubwa la Westgate jijini Nairobi.
Rais Kenyatta alibainisha vifo hivyo katika hotuba yake aliyoitoa kupitia televisheni usiku wa kuamkia jana, iliyolenga kuwapa pole Wakenya wote waliopoteza ndugu Hata hivyo, Kenyatta hakutaja majina ya ndugu zake waliopoteza maisha. Katika shambulio hilo lililohusisha matumizi ya maguruneti na risasi, watu takriban 59 waliuawa na kuacha majeruhi 175. Kikosi cha wanamgambo wa Al-Shabaab kimekiri kuhusika.
Ndani ya jengo hilo lililopo kilomita 10 Kaskazini Mashariki mwa kitovu cha Jiji la Nairobi, alikuwepo pia mtoto wa kiume wa Kenyatta, Jomo Kenyatta na dada wa Kenyatta, Kristina Pratt ambao waliokolewa bila majeraha yoyote.

Pia Kenyatta alitumia fursa hiyo kuwatoa hofu wananchi  juu ya shambulio hilo kubwa kuwahi kutokea nchini humu baada ya lile la kulipuliwa kwa Ubalozi wa Marekani na kikundi cha kigaidi cha Al-Qaeda mwaka 1998 lililoua watu 32.
“Tulishawahi kukumbana na mashambulio ya kigaidi hapo awali. Tulipigana kishujaa bila kuchoka na tuliushinda ugaidi nje na ndani ya mipaka yetu. Wakati huu pia tutawashinda. Ugaidi kwa kifupi ni falsafa ya woga,” alisema Kenyatta katika hotuba yake ya kwanza kuhusu shambulio hilo la kigaidi.

Hadi kufikia jana jioni, Serikali ilikuwa haijatoa idadi kamili ya mateka wanaoendelea kushikiliwa na wanamgambo hao wanaokadiriwa kuwa kati ya 10 na 15 ambao bado wapo ndani ya jengo hilo.
CHANZO: MWANANCHI

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...