Monday 30 December 2013

RAIS KIKWETE, DK SHEIN WAKABIDHIWA RASIMU YA PILI YA KATIBA MPYA

Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba akimkabidhi Rais Jakaya Kikwete (kulia) Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya leo.
Jaji Warioba akimkabidhi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.AliMohamed Shein (kushoto) Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya leo.
Rais Jakaya Kikwete (kulia) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba.


Jaji Warioba akisoma ripoti ya Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya leo.
Rais Jakaya Kikwete akihutubia wakati wa hafla hiyo.
Dk. Shein naye akihutubia katika hafla hiyo ndani ya Viwanja vya Karimjee, jijini Dar.
Bendi ya polisi ikitumbuiza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar..
Spika wa Bunge, Anne Makinda (kulia) akisalimiana na mmoja wa waalikwa.
Msajili wa vyama vya siasa nchini, Jaji Francis Mutungi (kushoto) akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Francis Mbatia (katikati) na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (kulia).
IGP Said Mwema katika hafla hiyo ndani ya Viwanja vya Karimjee jijini Dar.
Rais Kikwete wakati akiwasili Viwanja vya Karimjee.
Jaji Warioba akimkaribisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi.
Baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wakifuatilia hafla hiyo.
Waziri wa Afrika Mashariki Mh Samwel Sitta (mwenye chupa ya maji) akiteta jambo waalikwa.
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba leo amekabidhi Rasimu ya Pili ya Katiba Mpya  kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein katika hafla fupi iliyofanyika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
Hafla hiyo imehudhuria na viongozi mbalimbali wakiwemo wa vyama vya siasa, mawaziri, wabunge na baadhi ya wananchi walioalikwa.
Mheshimiwa Rais Kikwete ameagiza Rasimu hiyo ya Pili ya Katiba Mpya isambazwe kwenye mitandao ili kila Mtanzania aweze kuipata.
(PICHA ZOTE NA HARUNI SANCHAWA / GPL)

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...