Friday 31 January 2014
TIBA MBADALA: Kunywa maji ya moto ni tiba ya magonjwa mengi
Kuna tiba nyingi za kitabibu, zilizogawanyikaa katika makundi mbalimbali. Kuna zile za hospitali ambazo ni lazima zinunuliwe, lakini kuna tiba ambazo kwa ushauri wa daktari hata wewe unaweza kuziandaa bila kutumia gharama kubwa.
Moja ya tiba hizo ni kunywa maji ya moto. Kwa mujibu wa wataalamu wa afya maji moto yanatibu magonjwa mengi ikiwemo: Figo, kutoa sumu mwilini, kuyeyusha mafuta tumboni, kurahisisha mzunguko wa damu, kuondoa sumu kwenye ubongo na kusafisha haja ndogo.
Thursday 30 January 2014
NMB YADHAMINI MKUTANO WA TAASISI ZA KILIMO AFRIKA MASHARIKI
Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha biashara ya Kilimo NMB, Robert Pascal (pili kushoto) alipotembelea banda la NMB katika maonyesho ya Taasisi zinazojishughulisha na kilimo. Maonyesho haya yameshirikisha wadau mbali mbali kutoka Afrika Mashariki. NMB ikiwa ni miongoni mwa wadau wakubwa wa Kilimo nchini
Wednesday 29 January 2014
Tuesday 28 January 2014
SHULE YA SEKONDARI NAKAYAMA WAPOKEA TABULETI 61 TOKA OPPORTUNITY EDUCATION FOUNDATION
Serikali inakusudia kutoa maelfu kwa maelfu ya tabuleti za kufundishia masomo mbali mbali kwa wanafunzi na walimu wa shule za sekondari nchini kama njia ya ubunifu zaidi, ya kisayansi na ya uhakika ya kukabiliana na changamoto zinazoikabili sekta ya elimu kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT).
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokea akipokea moja ya Tabuleti 61 kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Wama Nakayama iliyoko kijijini Nyamisati, Rufiji, Mkoa wa Pwani toka kwa Mwenyekiti wa taasisi ya kusaidia elimu ya Opportunity Education Foundation wa Marekani Bw. Joe Ricketts wakati alipomtembelea Ikulu Jumapili Januari 27, 2014
Mwenyekiti wa taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi Dkt Shukuru Kawambwa, Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya WAMA Nakayama Dkt Ramadhani Dau na Mkuu wa Shule hiyo wakipokea moja ya Tabuleti 61 alizozitoa kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Wama Nakayama iliyoko kijijini Nyamisati, Rufiji, Mkoa wa Pwani Januari 27, 2014 toka kwa Mwenyekiti wa taasisi ya kusaidia elimu ya Opportunity Education Foundation wa Marekani Bw. Joe Ricketts .
Monday 27 January 2014
PICHA: BAADHI YA WASANII WALIOTUMBUIZA KATIKA GRAMMY AWARDS 2014
Beyonce na Jay Z wakitumbuiza katika sherehe za Grammy awards 2014,usiku wa jana
Watumbuizaji kutoka kushoto, Macklemore, Mary Lambert, Madonna, Ryan Lewis na Queen Latifah appear wakitumbuiza wimbo uitwao "Same Love" katika tuzo za Grammy 2014 jana
Mwanamuziki Steve Wonder nae alitumbuiza katika Grammy Awards 2014 |
PICHA: BAADHI YA TASWIRA KATIKA TUZO ZA GRAMMY AWARDS 2014,JAN 26, LOS ANGELES
Madonna, kulia ndani ya suti ya Ralph Lauren, akiwa na mwanae David Ritchie katika sherehe za GRAMMY Awards zilizofanyika katika Staples Center jumapili, Jan. 26, 2014, mjini Los Angeles. Beyonce Ciara Alicia Keys |
Sunday 26 January 2014
STANISLAS WAWRINKA ATWAA KOMBE LA MASHINDANO YA WAZI YA TENISI YA AUSTRALIA 2014
Stanislas Wawrinka ametwaa kombe la mashindano wa wazi Australia 2014 baada ya kumshinda mchezaji namba moja wa tenisi duniani Fafael Nadal, jijini Melbourne,Australia.Katika mchezo huo Rafa kama anavyoitwa na wengi,alipata majeraha ya mgongo yaliyomfanya kucheza chini ya kiwango.
Wawrinka alimshinda Rafa kwa 6-3 6-2 3-6 6-3.
Wizara yakemea ukatili na mauaji ya wanawake Butiama, Mara
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII JINSIA NA WATOTO
WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII JINSIA NA WATOTO
Hivi karibuni kumekuwa na taarifa za kutisha katika Wilaya ya Butiama mkoa wa Mara ambapo imearifiwa baadhi ya wanawake kuuawa kikatili kwa kukatwa vichwa.
Sababu ambazo hazijathibitishwa zinaeleza kuwa chanzo cha mauaji hayo ni pamoja na imani za kishirikina, uchu wa kumiliki mali, kulipiza visasi na kuendekeza hulka ya ukatili kwa kudhani kuwa mhusika anapata heshima yoyote katika jamii.
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kuwepo kwa mauaji hayo ya
Sababu ambazo hazijathibitishwa zinaeleza kuwa chanzo cha mauaji hayo ni pamoja na imani za kishirikina, uchu wa kumiliki mali, kulipiza visasi na kuendekeza hulka ya ukatili kwa kudhani kuwa mhusika anapata heshima yoyote katika jamii.
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kuwepo kwa mauaji hayo ya
kikatili na inawataka wananchi kutoa ushirikiano thabiti ili kuhakikisha kuwa matukio hayo ya udhalimu YANAKOMA MARA MOJA.
Saturday 25 January 2014
Friday 24 January 2014
MAMA SALMA KIKWETE AANDAA SHERRY PARTY KWA WAKE WA MABALOZI WA NCHI ZA NJE WAISHIO HAPA TANZANIA
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa hotuba yake wakati wa sherehe ya kuukaribisha mwaka mpya (sherry party) aliyowaandalia wake wa mabalozi wa nchi za nje walioko hapa nchini. Sherehe hiyo ilifanyika Ikulu tarehe 23.1.2014.
Kiongozi wa Umoja wa wake wa mabalozi waliopo hapa Tanzania Mama Celine Mpango, (ambaye ni Mke wa Balozi Juma Mpango wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo) akitoa salamu zake kwa niaba ya wanajumuia hiyo wakati wa sherehe hiyo iliyofanyika Ikulu Tarehe 23.1.2014.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA "READ MORE"
Subscribe to:
Posts (Atom)
PALM TREES ARE BEAUTIFUL
Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...
-
Dar es Salaam: Mwekezaji Sheikh Salim Abdullah ametangaza kuwekeza kwenye Uwanja Wa Ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere Dar es Salaam (JN...