Friday 8 May 2015

MAKALA: ADHA YA MAFURIKO DAR, HII IMEKAAJE WADAU?


Picha: GPL

Mvua zinazonyesha kwasasa nchini hususan jijini Dar zimeleta madhara mengi kubwa likiwa ni mafuriko.Mbali ya kuwa sababu kubwa ni wakazi waliojenga katika maeneo yasiyostahili,yakiwemo katika mikondo ya maji, kuna uzembe mwingine mkubwa pia.Uzembe huu ni mitaro ya kupitisha maji ambayo imeziba. 


Kuziba kwa mitaro  kwa upande mmoja ni uzembe wa wananchi,ambao kwa upande wao hutupa takataka ovyo,katika maeneo yasiyo rasmi. Kwa upande wa pili ni wahusika na uangalizi wa mitaro hiyo na wale walioitengeneza(sijui ni halmashauri ya jiji au nani).Kwanini basi?
Sababu ni hii; mitaro mingi haijazibwa iko wazi tu.Sidhani kama mitaro ya kupitisha maji inatakiwa kuwa hivi.Kwa kuiacha wazi ndiyo kunachangia wananchi kujitupia ovyo tu takataka.Athari hizi hazionekani wakati wa kiangazi bali ndiyo haya tunayoyaona nyakati za mvua.Kwa mtazamo wangu, ni kosa vilevile kwa wahusika kuanza kusafisha mitaro wakati mvua zikiwa zimeshaanza.Walikuwa wapi kabla?
Kila mtu awajibike katika eneo /jukumu lake na haya hayatatokea.Ni hayo tu!

Wewe mdau una lipi la kuchangia?

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...