Kamishna Mkuu wa idara ya Uhamiaji anatangaza nafasi za kazi katika Idara ya Uhamiaji kwenye
vyeo vya Koplo na Konstebo wa uhamiaji.
A: MKAGUZI MSAIDIZI WA UHAMIAJI NAFASI 70
1. SIFAZINAZOHITAJIKA
Awe na shahada ya kwanza au Stashahada ya juu kutooka vyuo vikuu vinavyotambuliwa na serikali katika fani zifuatazo; Sheria, Uchumi, Biashara, Utawala, Uandishi wa habari, Ualimu, Usafirishaji, Rasilimali watu, Sayansi ya kompyuta, Teknolojia ya mawasiliano, Takwimu, Uchapaji, Uhandisi majengo na Uhandisi Mitambo.
Awe na umri usiozidi miaka 35
2. MAJUKUMU NA KAZI ZA KUFANYA
(i) Kusimamia doria sehemu za mipakani, Bandarini, Vituo vya Mabasi, Treni na sehemu zenye vipenyo vya kuingia na kutoka nchini vikiwemo vya majini.
(ii) Kusimamia shughuli za upelelezi, kuandaa hati ya mashitaka na kuendesha mashitaka.