Showing posts with label CHAKULA. Show all posts
Showing posts with label CHAKULA. Show all posts

Thursday, 18 September 2014

MWILI HAUJENGWI KWA MBAO

Leo ni kinyumbani zaidi . Nimepika ugali, bamia (mlenda)na dagaa.Nk vitamuje sasa! Karibuni kwa picha.

Friday, 5 September 2014

VIUNGO 10 AMBAVYO NI LAZIMA KUWA NAVYO JIKONI KWANGU,JE WEWE VYAKO NI VIPI?



1.     PASTA
 Hiki ni chakula cha haraka.Unaweza kutayarisha pasta kwa kuongeza tu protini ulizonazo katika jokofu lako mfano kuku,nyama ya kusaga, kamba(prawns) n.k.Ili kuzifanya pasta zako ziwe tamu  pasha  ½ kikombe cha  mafuta ya zeituni(olive oil) kikaangoni,weka spinachi,nyanya au uyoga.Pika kwa dakika 3 au mpaka mboga zilainike. Ongeza chumvi na pilipili(kama unatumia pilipili).Changanya pasta zako ambazo zimepikwa tayari katika mchanganyiko huu wa mboga.

2.  CHICKEN BROTH OR BOUILLON
 Unaweza kutengeneza mchuzi au supu kwa kutumia chicken broth pamoja na viungo vingine ulivyonavyo jikoni kwako na kupata mlo mzuri kabisa. Mfano unaweza kuongeza mbogamboga au nyama nk.Unaweza kutumia hii katika kuongeza ladha kwenye kuku wa kuoka,kupikia wali na hata mbogamboga badala ya kutumia maji.

Friday, 18 April 2014

SUPU YA UYOGA KWA CHAPATI,NI TAMUJE!



Hii ni supu ya uyoga ambayo unatumia dakika kama 5 hivi kutayarisha.Ni supu ambayoinatokana na  unga uliomo katika pakiti na unafuata maelekezo tu kutengeneza.Mimi hupendelea kuila na chapati.Ni mlo wa haraka kwa kweli.Chapati nakuwa nimetengeneza tayari hivyo ndani ya dakika 10 mlo huu huwa tayari. Hula mlo huu kama mlo wa kati.Ndiyo mlo wa kati niliokula leo!

Tuesday, 17 September 2013

AINA MBALIMBALI YA MBOGA ZA MAJANI

Zijue baadhi ya aina tofauti ya mboga za majani.Mboga za majani ni muhimu sana katika afya zetu.Siku zijazo nitawaandikia jinsi ya kupika aina mbalimbali ya mboga za majani hivyo usiache kutembelea hapa.
Mchicha

Matembele
Majani ya maboga

Kisamvu

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...