Sunday 30 June 2013

NGUO ZA OUTING WADAU

Mermaid V-neck Floor-Length Taffeta Evening Dress With Ruffle Flower(s) (017002546)A-Line/Princess Sweetheart Asymmetrical Chiffon Evening Dress With Ruffle Beading (017017379)

A-Line/Princess One-Shoulder Floor-Length Chiffon Evening Dress With Ruffle (017025590)A-Line/Princess One-Shoulder Knee-Length Chiffon Cocktail Dress With Ruffle Beading (016008400)

HABARI KATIKA PICHA:OBAMA AKIWA ROBBEN ISLAND




Gereza la Robben


Rais Obama na mkewe Michelle wakitembea katika gereza la Robben karibu na  mji wa Cape town.
President Barack Obama and First Lady Michelle Obama in a prison yard at Robben Island, 30 June 2013



MAMA SALMA KIKWETE KWENYE MKUTANO WA SMART PARTNERSHIP 2013.

IMG_1282
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza na Rais wa Sri Lanka Mheshimiwa Mahinda Rajapaksa wakati wa mkutano wa smart partnership dialogue 2013 unaofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere hapa Dar es Salaam kuanzia tarehe 28.6.2013. IMG_1322
Rais Jakaya Kikwete akifurahia jambo na Mfalme Mswati wa Swaziland na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Ndugu Benard Membe wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa na Rais Kikwete kwa Marais na wajumbe wa mkutano wa smart partnership unaofanyika Dar es Salaam kuanzia tarehe 28.6 hadi 30.6.2013. IMG_1425
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo Mama Salma Kikwete akijiandaa kuzungumza na wake wa Marais na Wakuu wa nchi wakati wa mkutano wa smart partnership tarehe 29.6.2013 kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere hapa Dar es Salaam.  IMG_1437
Baadhi ya wake wa viongozi mbalimbali wanaohudhuria mkutano wa smart partnership wakimsikiliza Mama Salma Kikwete (hayupo pichani) wakati akizungumza nao kwenye ukumbi wa Mwalimu Nerere tarehe 29.6.2013.
IMG_1454
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa pamoja na Mke wa Mfalme wa Mswati wa Swaziland, Inkhosikati Lambikiza (kushoto), na Mwakilishi wa Mke wa Rais Joseph Kabila wa DR Congo (kulia) wakimwalika Mke wa Makamu wa Rais wa Zambia Mama Charlotte Scott (hayupo pichani) kujiunga nao katika picha ya pamoja mara baada ya kikao chao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Mwalimu Nyerere tarehe 29.6.2013. IMG_1458
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wake wa Marais na Wakuu wa nchi wanaohudhuria mkutano wa smart partnership unaofanyika hapa Dar es Salaam. Kutoka kushoto no Mama Charlotte Scott, Mke wa Makamu wa Rais wa Zambia akifuatiwa Inkhosikati Lambikiza, Mke wa King Mswati, Mama Salma Kikwete,  akifuatiwa na Mama Siti Hasma, Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu wa Malaysia Mahathir Mohammed na kulia ni mwakilishi wa Mke wa Rais wa DR Congo.
IMG_1486
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiaagana na Mama Siti Hasma mara baada ya kuhudhuria kikao cha wake wa marais na wakuu wa nchi kwenye mkutano wa smart partnership. IMG_1577
Mke wa Rais akiwa katika picha ya pamoja na Inkhosikati Lambikiza wa Swaziland.
IMG_1631
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiagana na Mama Charlotte Scott
 IMG_1783_1
Mama Salma Kikwete na Inkhosikati Lambizana wakijiandaa kwenda katika chakula cha usiku kilichoandaliwa kwenye ukumbi wa mkutano wa Mwalimu Nyerere.
Waziri Mkuu wa Malaysia Mheshimiwa Najib Razak akiwa pamoja na Mama Salma Kikwete na Inkhosikati Lambizana wakimwangalia simba dume aliyewekwa nje ya ukumbi wa  jengo la mikutano la Mwalimu Nyerere baada ya viongozi hao kuhudhuria chakula cha usiku tarehe 29.6.2013.
IMG_1842
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiaagana na Mfalme Mswati wa Swaziland mara baada ya chakula cha usiku. IMG_1852
Rais Jakaya Kikwete akiiagana na Waziri Mkuu wa Malaysia Mheshimiwa Najib Razak mara baada ya viongozi hao kupata chakula cha usiku kwenye ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere tarehe 29.6.2013.
PICHA NA JOHN  LUKUWI

OUTDOOR FUNITURE








Rattan Garden Furniture Set



OBAMA...OBAMA



  • Rais wa Marekani Barack Obama 


  • Kutua Dar kesho... Jiji lazizima mabango ya kumkaribisha kila kona
    Ulinzi wazidi kuimarishwa, askari wa JWTZ wahusika
    Hekaheka zimetanda jijini Dar es Salaam,ikiwa ni zaidi ya saa 24 kabla ya kuwasili kwa Rais Barack Obama.
    Rais Obama, atawasili nchini kesho akitokea Afrika Kusini, ambapo pamoja na mambo mengine, alizungumza katika mkutano wa ‘viongozi vijana wa Afrika’ na kujibu maswali kutoka nchi tofauti.
    Mkutano huo ulifanyika jana jioni huko Soweto nchini Afrika Kusini, ambapo alipokewaa na kujibu maswali kutoka Kenya, Uganda, Nigeria na Afrika Kusini kwenyewe.

    Jijini Dar es Salaam, shughuli kadhaa zikiwamo za ulinzi na usalama, zinafanyika kwa kasi na umakini kuhakikisha ziara ya Rais Obama inafanyika pasipo bughudha. kujibu maswali kutoka Kenya, Uganda, Nigeria na Afrika Kusini kwenyewe.
    Jijini Dar es Salaam, shughuli kadhaa zikiwamo za ulinzi na usalama, zinafanyika kwa kasi na umakini kuhakikisha ziara ya Rais Obama inafanyika pasipo bughudha.
    Hata hivyo, sehemu kubwa inayohusu masuala ya itifaki, ulinzi na usalama yanafanywa na taasisi za Marekani, kwa kuzishirikisha taasisi za ndani kwa kiwango kidogo.
    “Hawa jamaa (Wamarekani) wanapoingia nchi yeyote wakiwa na Rais wao, shughuli nyingi na uamuzi wanafanya wao, sisi wa ndani inakuwa kushirikishwa kwa kiasi kidogo,” kilieleza chanzo cha NIPASHE Jumapili kutoka moja ya taasisi zinahusika katika ziara hiyo.

    KATUNI: NIMEIPENDA HII



    MASANJA NA SHILOLE WAELEKEA WASHINGTON,DC KWENYE SHEREHE YA MIAKA 3 YA VIJIMAMBO NA TAMASHA LA UTAMADUNI WA KISWAHILI.

    278
    Wasanii Masanja Mkandamizaji na Shilole wakikwea pipa kuelekea Washington, DC kwenye sherehe ya miaka 3 ya Vijimambo na Tamasha la Utamaduni wa Kiswahili Marekani litakalofanyika July 6, 2013 kuanzia saa 4 asubuhi (10:00 am) na Rais Mustaafu Ali Hassan Mwinyi ndiye atakayekua mgeni wa rasmi. Mhe. Ali Hassan Mwinyi anatarajiwa kufika Washington, DC siku ya Alhamisi July 4, 2013.
    PICHA KWA HISANI YA Mo blog

    RAIS KIKWETE AWAANDALIA MARAIS DHIFA YA KITAIFA YA CHAKULA CHA USIKU


     Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Mfalme wa Swaziland, King Mswati katika hafla ya chakula cha usiku alichokiandaa kwenye viwanja vya Gymkhana, Dar es Salaam jana usiku, kwa waliohudhuria Mdahalo wa Kimataifa wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia kwa Manufaa ya Wote (Global Smart Partinership Dialogue). TBL ni moja kati kampuni zilizofadhli hafla hiyo.
     Mahali palipoandaliwa kwa dina kwenye viwanja vya Gymkhana
     Rais wa zamani wa Msumbiji, Joachim Chisano (kushoto) akikaribishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernald Membe katika hafla ya chakula cha usiku.
     JK akiwa na Museveni wa Uganda (kushoto), Kingi Mswati wa Swaziland na Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi

    Saturday 29 June 2013

    ZIARA YA OBAMA AFRIKA YA KUSINI KATIKA PICHA



    Rais Obama kushoto na Michelle kulia wakikaribishwa na Jacob Zuma na mkewe Tobeka latika jumba la Umoja,Pretoria



    Rais  Barack Obama na mkewe  Michelle Obama,kushoto, akipunga.Wa pili kulia ni rais wa Afrika ya kusini  Jacob Zuma, na mkewe Tobeka Madiba Zuma, kulia, katika ngazi za jengo la Umoja lililopo Pretoria, Afrika ya kusini,Jumamosi juni 29.

    DUNIANI KUNA MAMBO:ASHURA MACHUPA AELEZEA ALIVYOKWENDA KWA MGANGA ILI AWE SUPERSTAR KWENYE TAARAB-LIVE

    WAZIRI MKUU MHE. MIZENGO PINDA NA MATUKIO BAADA YA KUAHIRISHA BUNGE MJINI DODOMA

    IMG_0551Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Spika wa Bunge, Anne Makinda baada ya kuashirishwa kwa kikao cha Bunge Mjini Dodoma Juni 28, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)IMG_0673Spika wa Bunge Mama Anne Makinda akizungumza na mke wa Waziri  Mkuu, Mama Tunu Pinda kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 28,2013. (Picha na Ofisi ya Wairi Mkuu)IMG_0700Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mkewe Tunu wakizungumza na Spika wa Bunge Mama Anne Makinda   (katikati)  kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 28,2013. (Picha na Ofisi ya Wairi Mkuu)IMG_0569Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akipongezwa na mkewe   Tunu  kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 28,2013 baada ya hotuba yake ya kuahirisha kikao cha Bunge Mjini  Dodoma . (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

    NMB YAENDELEA KUZINDUA BUSINESS CLUB “SASA NI ZAMU YA KARATU”

    P1650255Mhandisi mkuu wa Wilaya ya Karatu, Tulinumpoki Mwakalukwa akitoa shukrani zake kwa NMB mara baada ya kuzindua rasmi  NMB Business Club wilaya ya Karatu. Kushoto ni Meneja wa NMB tawi la Karatu , Evarist Mtaro na mkuu wa kitengo cha wajasiliamali wadogo wadogo na wakati wa NMB Filbert  Mponzi.
    ………………………………………………………..
    Benki ya NMB imeendelea kuwa kinara katika kubuni na kuboresha huduma mbali mbali za kibenki, ili kuwawezesha wateja wake kupata unafuu na urahisi wa upatikanaji wa huduma za kibenki nchini Tanzania.
    Katika kulizingatia hili, NMB imezidi kuzindua klabu maalum za wafanyabiashara maarufu kama NMB Business Club. Hadi sasa zaidi ya NMB Business Club 29 zimekwisha zinduliwa nchi nzima.
    Kupitia NMB Business Club wajasiliamali wanaowezeshwa na benki ya NMB wamekua wakipata nafasi ya kujifunza jinsi ya  kuandika michanganuo ya biashara zao na pia kuendelea kua vinara wa biashara.
    P1650470Mkuu wa kitengo cha wajasiliamali wadogo wadogo na wakati wa NMB ,Filbert  Mponzi akimkabidhi mwenyekiti wa  NMB Business Club Paulith Jack  mara tu baada ya kuibuka kidedea kwenye mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa NMB Business Club Karatu .
    P1650350Sehemu ya wanachama wa NMB Business Club wilaya ya Karatu wakifurahia uzinduzi wa NMB Business Club.
    CHANZO:Full shangwe

    KIKWETU KWETU NA AFRICAN PRINT DRESSES!











    PALM TREES ARE BEAUTIFUL

    Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...