| Mtoto Nasra,enzi ya uhai wake. |
Mtuhumiwa no.1:Rashid Mvungi,baba Mtuhumiwa no.2: Mariam Said,
wa Nasra mama mlezi
Mtuhumiwa wa tatu, Mtonga Omar, baba mlezi wa Nasra
Kutokana na kifo cha
kusikitisha cha motto Nasra naomba tujadiliane.
Hivi hawa waliomfanyia ukatili mtoto Nasra Mvungi,”maarufu
kama mtoto wa boksi ”wapewe adhabu gani?Tukumbuke mwanzo walishatakiwa
kwa kutuhumiwa kumfanyia mtoto Nasra ukatili. Kwasasa mtoto Nasra amefariki
kutokana na madhara aliyoyapata kutokana na ukatili wa kupitiliza aliofanyiwa. Kwanza, natumaini mashtaka yao
yatabadilishwa na kuwa mauaji.Je, wewe mdau unayesoma hapa,ungefarijika kama
watu hawa wangepewa adhabu gani? Je,tunahitaji watu kama hawa kwenye jamii
yetu?
Hapo ulipo,hakuna mtu / watu wanaofanyia watoto/ mtoto ukatili
unaofanana na huu?Kama wapo,umefanyanini kusaidia?
Je, unataka kumuenzi vipi mtoto Nasra?
CHUKUA
HATUA ILI KULINDA UHAI WA WATOTO.
Na Anna Nindi
No comments:
Post a Comment