Sunday 23 June 2013

SNOWDEN ATUA MOSCOW

Edward Snowden

Ndege iliyombeba mtaalamu wa zamani wa shirika la ujasusi la Marekani, Edward Snowden imetua mjini Moscow baada ya kusafiri kutoka Hong Kong.

Chanzo kutoka ndege hiyo ya taifa la Urusi kimesema bwan snowden anayetakiwa na Marekani kwa mashtaka ya wizi wa siri za serikali,
Amepanga kuondoka hapo kesho jumatatu kuelekea nchini Cuba kabla ya kuelekea Venezuela ambako amepanga kuomba hifadhi.
Mamlaka ya Hong Kong imesema bwana Snowden aliondoka kwa hiyari yake mwenyewe na kisheria baada ya kugundua njama za kutaka kumkamata zinazofanywa na mtandao wa kijasusi wa marekani kambi ya Uchina.
Hong Kong imesema imeyakataa maombi ya marekani ya kutaka kumkamata na kumrejesha bwana Snowden nchini Marekani kwa nguvu kwa kuwa maombi hayo hayaendani na sheria za ndani za nchi hiyo.
CHANZO: BBC

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...