Friday 28 June 2013

UHISPANIA KUCHUANA NA BRAZIL

Wachezaji wa Uhispania
Wachezaji wa Uhispania wakisherehekea baada ya kufuzu kwa fainali ya kombe la Shirikisho
Mabingwa wa kombe la dunia Uhispania watachuana na Brazil katika fainali ya kombe la Shirikisho siku ya Jumapili baada ya kuishinda Italia katika mechi ya nusu fainali kupitia kwa mikwaju ya penalti.
Uhispania ilijikatia tikiti ya fainali hiyo kwa kuilaza Italia kwa magoli saba kwa sita mjini Fortaleza.
Mchezaji wa akiba Jesus Navas, ndiye aliyeifungia Uhispania bao lake la ushindi baada ya mlinda lango wa Italia Leonardo Bonucci kupoteza zamu yake.
Katika dakika tisini za kawaida, Italia ilionekana kutawala mechi hiyo, lakini juhudi zao ka kufunga ziliambulia patupu.
Katika muda wa ziada mkwaju wa Emanuele Giaccherini, uligonga mlingoti wa goli la Uhispania naye Gianluigi Buffon alizuia mkwaju wa Xavi Alonzo na kuifanya ugonge pia mlingoti wa goli.
Navas ambaye anajiunga na Manchester City msimu ujao alifunga bao la mwisho na kuhakikisha kuwa mabingwa hao wa dunia wanachuana na wenyeji wa mashindano hayo Brazil ambao walishinda mechi yao ya nusu fainali dhidi ya Uruguay kwa magoli mawili kwa moja siku ya Jumatano.


Jesus Navas
Jesus Navas

Italia sasa itachuana na Uruguay kutafuta mshinda wa tatu na nne siku hiyo hiyo ya Jumapili.

CHANZO: BBC

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...