MSANII nyota wa filamu Bongo Wema Isack Sepetu amefunguka kwa kudai kuwa hawezi kuachana urafiki na meneja wake Martin Kadinda kwa sababu kama kuna kitu chochote cha mafanikio nyuma yake yupo Kadinda jambo anasema hana rafiki aliye wa karibu kuliko meneja huyo ambaye amekuwa akimuongoza vema.
“Kadinda ndiye kila kitu kwangu, hata akiondoka na kukaa mbali na mimi kwa muda mrefu ninapokutana naye tu, nitamweleza kila kitu toka siku ya mwisho tuliyoachana hivyo inakuwa kama sijapoteana naye ni kama vile nipo naye kila siku iendayo kwa Mungu,”anasema Wema.
Msanii huyu ameendelea kusema kwamba hata kampuni yake ya Endless Fame film alifungua kwa msaada wa Kadinda baada ya kumshauri kwa hadhi yake anastahili kuwa na kampuni na kuachana kuigiza filamu za watu wengine.
CHANZO: FILAMU CENTRAL
No comments:
Post a Comment