Thursday 20 March 2014

HOJA: NINI KINAVUNJA NDOA NYINGI SIKU HIZI?


Masiah ya ndoa siku hizi yanasemekana kuwa na changamoto nyingi sana
Kuvunjika kwa ndoa ni jambo ambalo katika jamii nyingi za kiafrika lilikuwa gumu kutokana na misingi ya tamaduni na mila ambazo zilikuwa na mbinu za utatuzi wa migogoro na kuhakikisha wanandoa hawaachani.


Lakini kadri ya miaka inavyozidi kwenda mbele inaonekana ni rahisi wanandoa kufikia hatua ya kutamkiana wazi kuwa sasa basi na kweli inakuwa basi.

Wazee walioishi chini ya mila na desturi za zamani wanakosoa mfumo wa ndoa uliopo sasa na kudai kuwa mifumo yao ya kale ilikuwa mizuri. Kwa nini Ndoa zinavunjika kwa urahisi siku hizi?Je mifumo ndio mibaya au?
CHANZO: BBC

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...