Sunday 8 June 2014

MSICHANA ANG’ATWA NA KUCHOMWA NA PASI NA MWAJIRI WAKE





Hali ya msichana Yusta Lucas mwenye umri wa miaka 20  aliyefanyiwa ukatili  wa kufungiwa  ndani kwa zaidi ya mwaka mmoja huku akipewa adhabu ya kunga'twa na kuchomwa kwa pasi  na mwajiri wake Amina Maige wa Mwananyamala jijini Dar es salaam inaendelea vizuri  kufuatia matibabu  anayopata ya  majeraha yaliyomsababisha kupoteza fahamu.


ITV imefika katika hospitali ya Mwananyamala alikolazwa binti huyo mzaliwa wa Tabora na kuweza kufanya nae mahojiana ambapo akiongea kwa tabu amesema alianza kuishi na mwajiri wake tangu mwaka 2011 bila kuruhusiwa kutoka nje ya njumba waliyokuwa wanaishi ama kuwasiliana na ndugu zake na hata kurudi kwao ambpo mwajiri wake huyo alifiki kipindi akabadilisha adhabu pindi anapofanya makosa na kumwadhibi kwa kumuuwa kwa meno yake na kumchoma kwa pasi na maji ya moto.
Mganga mfawidhi hospitali ya mkoa Mwananyamala amesema hali ya binti huyo inaendelea kuimarika baada ya kuanza kupewa matibabu na kubaini tayari alikuwa ameshaadhirika kisaikolojia kiasi cha kuogopa hata kuangalia watu kutokana na kutoanana na watu kwa muda mrefu.

Mkaguzi msaidizi wa polisi dawati la jinsia Prisca Komba amesema walifanikiwa kujua mateso ya binti huyo baada ya kupewa taarifa na msamaria mwema ambaye alikuwa jirani yake na kuwa uchunguzi bado unaendelea wakati mtuhumiwa akiwa bado rumande na kutoa wito kwa jamii kuendelea kuibua matukio kama hayo ili watuhumiwa waweze kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.


Afisa programu kituo cha sheria na haki za binadamu bi Naemy Sillayo amaesema wao kama kituo cha kutetea haki za binadamu wameendelea kusikitishwa na vitendo vinavyotokea hapa nchini na kutoa wito kwa jamii kuviibua.
CHANZO: ITV

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...