Sunday 12 October 2014

NASI GORENG: KILE CHAKULA NILICHOANDAA JANA USIKU!

Wasomaji wangu.Katika jikoni kunani jana niliweka vionjo vya chakula nilichokuwa naandaa na nikawaahidi nitaleta picha ya mwonekano wake mwisho.Hii si pilau kama inavyoonekana bali ni chakula kiitwacho "Nasi Goreng"


Ni mchanganyiko wa wali uliopikwa, vitunguu maji (kata vipande vidogovidogo), kabichi iliyokatwa vipande vidogo wastani kiasi kidogo, pilipili hoho nyekundu 1, pilipili hoho kijani 1, unga wa binzari vijiko 4 vya chai, unga wa pilipili hoho nyekundu vijiko 3 vya chai, soya sosi vijiko 2 vya chai, mafuta ya kupikia vijiko 4 vya chakula(unawza kuongeza), chumvi kijiko 1 cha chai(unaweza kuongeza kwa ladha unayotaka), kitunguu swaumu, vipande vidogo vya steki kuku ya kukaanga au kuchoma gramu 400, njegere 1/2 kikombe na kamba gramu 100(prawns).

Mlo huu unafaa kuliwa na saladi.Ni mlo mzuri kwani una virutubisho vingi.

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...