Monday 23 March 2015

2. TEMBEA UONE: MAWASILIANO YA BARUA

Kopjes between Tunduru and Masasi

Safari moja nilikuwa nasafiri kikazi kutoka wilaya ya Tunduru kuelekea mtwara. Barabara ya Tunduru-Masasi ni moja ya barabara zilizokuwa mbaya sana.Sijui kwasasa iko vipi maana hiyo ilikuwa ni miaka 10 iliyopita. Tulikuwa katika landrover 110. Tulipita vijiji mbalimbali. Baada ya kwenda kwa muda,dereva wa gari yetu alisimama katika kijiji kimoja na kutupa barua pembeni mwa barabara. 


Barua hizo alizitia katika mfuko wa plastiki unaaonyesha. Mimi nilishangaa na kumuuliza dereva,alikuwa amefanyanini? Akaniambia,”dada,huku barua nyingi za wakazi wa vijiji hivi zinaletwa kwa namna hii na hakuna barua inayopotea labda itokee bahati mbaya. Mkazi yeyote wa kijiji akipita, anaokota barua na kuzifikisha kwa mhusika/wahusika. Na nimeziweka katika mfuko wa plastiki ili hata kama mvua itanyesha barua ziwe salama”. Kwa kweli nilishangaa sana ila nilifurahishwa kwa wakazi kuwa na utaratibu wao mzuri wa kuhakikisha kuwa umbali,ubovu wa miundo mbinu haukuwa kikwazo kwa wao kupata mawasiliano kutoka kwa jamaa zao n.k


KWELI TEMBEA UONE!

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...