Wednesday 25 March 2015

TEMBEA UONE: SALAM ILIYONITATIZA WILAYANI TUNDURU


                                                            Tunduru mjini
Nilipokuwa katika wilaya ya Tunduru kikazi nilikutana na salam ambayo ilinitatiza.Kweli tembea uone.
Ilikuwa ni asubuhi ya siku ya pili toka nifike wilayani Tunduru. Mmoja wa wafanyakazi wa hoteli niliyofikia alinisalimia, ”dada habari za mwili?”


Kwa kweli nilitoa macho kwanza na sikujua nimjibu nini. Nilijiuliza alikuwa na maana gani kuniulizia habari za mwili? Nikiwa ndani ya mshangao nilimjibu nzuri ila sikuwa na uhakika na jibu langu.
Baada ya jibu hilo akaniuliza tena, ”za muamko?” Hahaha
Nikasema leo nimepatikana. Nikamjibu, ”nzuri”. Ila kama jibu la kwanza, sikuwa na uhakika na jibu langu.
Nilipoenda kukutana na wafanyakazi wenzangu,niliwaelezea yaliyonikuta. Walicheka sana na kuniambia kuwa hiyo ilikuwa ni salam ya kawaida kabisa ya wakazi wa Tunduru.Na kuwa nilijibu sawa.
KWELI TEMBEA UONE.

Imeandikwa na Anna Nindi

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...