Saturday 11 April 2015

TEMBEA UONE: USHIRIKINA MAKAMBAKO







Nilitembelea Makambako,iliyopo mkoani Iringa.Nilikuwa na safari ya Makambako, Songea na Mbeya. Makambako pana baridi nyakati za jioni hasa katika kipindi nilichokwenda,mwezi wa agusti kama sikosei.Jua lilikuwa kali sana mchana.


Nikiwa Makambako nikapewa stori ya kutisha kidogo kuwa wamiliki wengi wa maduka pale Makambako,walikuwa wanatumia ushirikina kufanya biashara zao. Mojawapo ya ushirikina waliokuwa wanafanya ni mnunuzi unapokwenda dukani,basi mwenye duka atakuona ukiwa mtupu(ukiwa huna nguo).Je,walifanya hivi kwaajili ya nini? Jibu ni kuwa,kwa kufanya hivi walivutia wateja zaidi na kuuza zaidi.Niliogopa kwa kweli ila sikujua kama ni kitu cha kweli au la.
Nilijiuliza maswali mengi kuwa kwanini mtu afanye biashara kishetani namna hii? Je,wateja waliojua hili(kama ni kweli),walijisikiaje walipokuwa wakienda madukani? Jamani,ni stori niliyopewa na wenyeji,hivyo sina uthibitisho.

KWELI TEMBEA UONE

Imeandikwa na Anna Nindi

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...