Tuesday 14 April 2015

WANAWAKELIVE: VILIO VYA WANAWAKE WAJANE KUDHULUMIWA MALI WALIZOCHUMA NA WAUME ZAO



Nadhani ni wakati mwafaka wa kuwa na taasisi/vyombo vingi visivyo vya kiserikali ili kushughulikia maswala ya sheria za mirathi kwa wanawake wajane. Inasikitisha kuona mwanamke amechuma mali na mumewe kwa taabu ndugu za mume wakiwa na yao halafu anapofariki mume wao wanajileta kurithi mali.Mali ipi hapa? Jamani watu hawana aibu hivi. Marehemu kaacha mke na watoto wake na hao ndiyo warithi halali wa mali. Sasa hawa ndugu za mume wakichukua mali ambayo wala hawakuichuma,watoto wataishi vipi? Watu waache kubweteka na kusubiri mali za kurithi.
Nimeupenda ujasiri wa mwanamke wa mwisho katika video hiyo hapo juu.Yeye aliamua kukomaa na wapenda vya bure.Tuwasaidie wale wasioelewa haki zao.
Mwanaume jasiri hutafuta mali yake mwenyewe kwa jasho lake na mtegemea cha ndugu siku zote,hufa masikini.

Badilikeni!

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...