Tuesday, 4 June 2013

MWANAJESHI WA MAREKANI ANAYESHUTUMIWA KUTOA SIRI KWA TOVUTI YA WIKILEAKS KUFIKISHWA MAHAMANI

Manning Wikileaks
Mwanajeshi  wa  Marekani  anayetuhumiwa  kutoa  zaidi  ya nyaraka  700,000  za  siri  kwa  tovuti  ya  Wikileaks  anafikishwa mahakamani  leo (jana) mjini  Maryland  akishtakiwa  kwa  kuvujisha taarifa hizo  za  siri.
Kuruta wa  ngazi  ya  kwanza  Bradley Manning (pichani) mwenye  umri  wa  miaka  25, anakabiliwa  na  uwezekano  wa kifungo  cha  maisha bila  msamaha  iwapo  atapatikana  na  hatia kwa kuvujisha  nyaraka  hizo  mwaka  2010, hali  ambayo iliikasirisha  serikali  ya  Marekani.
Manning anakabiliwa  na  mashataka  21, ikiwa  ni  pamoja  na shitaka baya  zaidi  la  kusaidia  adui, pamoja  na  kukabiliwa  na hukumu  chini  ya  kifungu  cha kupambana  na  ujasusi  cha  mwaka 1917.
Mahakama  ya  kijeshi  ya  Fort Meade, Maryland , kiasi ya  kilometa  50  kaskazini  mashariki  ya  mji  wa  Washington, inatarajiwa  kuendesha  kesi  hiyo  hadi  karibu  mwishoni  mwa mwezi  August.

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...