Wednesday 25 March 2015

UPISHI WA BAMIA AU OKRA



MAHITAJI
½ kjc giligilani nzima
½ kjc jeera(binzari nyembamba) nzima
1 kitunguu maji-kata vipande vidogovidogo
1kjc chumvi


½ kjc unga wa giligilani
½ kjc unga wa jeera
¼ kjc binzari
½ kjc pilipili ya unga/tandoori masala
¼ kjc unga wa cayenne
Vikombe 4-5 bamia iliyokatwa katika duara ndogo
4-5 Nyanya –kata vipande vidogovidogo

4 KJ mafuta ya mizeituni(olive oil) au mafuta yeyote  ya kupikia uyapendayo.

FANYA HIVI 
Kaanga vitunguu na olive oil mpaka view rangi ya kahawia kwa mbali. Moto
 uwe wa mdogo wastani. Weka jeera na giligilani nzima  na kanga kwa dakika 1. Weka bamia na changanya vizuri. Funika na acha kwa dakika 2.
Ongeza chumvi, pilipili ya unga/taandori masala, jeera ya unga, giligilani ya unga, cayenne na binzari. Changanya vizuri na funika, acha iive kwa dakika 5-6 katika moto mdogo.
Mwisho,weka nyanya na pika kwa dakika 5. Bamia yako ni tayari.
Unaweza kula na wali, ugali n.k

MAANA YA VIPIMO VYANGU
kjc: Kijiko cha chai
KJ: Kijiko cha chakula

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...