Wednesday 8 April 2015

JUISI YA BUNGO

Hii ni moja kati ya juisi nizipendazo.Mabungo hulimwa  Zanzibar ila hupatikana Dar es salaam pia.

Tunda la bungo linavyoonekana. Hizi mbegu za ndani, zikichanganywa 
na maji,ndiyo hutengenezwa juisi.


MAHITAJI

Vipimo: Kupata takriban gilasi 6
3 Mabungo                                                    
6-7 glasi za maji                                                            
Sukari kiasi upendacho                                                       
*Chumvi kidogo sana   (Chumvi hukata uchachu)


Juisi ya bungo


FANYA HIVI
1.  Kata mabungo na toa mbegu zake na weka katika mashine ya kusagia.
2. Weka maji, sukari na chumvi usage kidogo tu.
3.  Chuja,mimina katika jagi weka katika friji.
4.  Mimina katika glasi na furahia juisi yako.
DOKEZO: Unaweza kunywa juisi ya bungo kwa kitafunwa upendacho au na mlo upendao.Ni nzuri sana ikinywewa ya baridi.


No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...