Wednesday 8 April 2015

MAKALA: ULANZI


Ugemaji wa ulanzi

Ulanzi ni pombe ambayo hugemwa kwenye vitindi, au kwa jina lingine kwenye mianzi midogo midogo ambayo haijakomaa, pindi tu inapochomoza kutoka ardhini baada ya siku chache. Ulanzi unapogemwa kwa mara ya kwanza huwa mtamu kama togwa au juisi, lakini unapomaliza siku mbili, tatu au nne, huwa mkali. Ulanzi ni pombe ya asili sana kwa wapangwa, maana ni jadi kwa wapangwa kunywa ulanzi. 


Ulanzi unavyoonekana (picha na riziki yetu blog)
Hata watoto wadogo hupewa ulanzi kama juisi. Ulanzi kwa wapangwa, ni pombe ambayo inaheshimika sana. 
Wapangwa wanapokwenda shambani, huenda na ulanzi, na kama ukimpeleka Mfanyakazi shambani bila ulanzi, huwa anakaidi kufanya kazi, hadi apewe ulanzi.
Pia, hata katika harusi, sherehe za kimila kama vile kujengea makaburi(MAHOKA), Mila za kumurudisha mjane nyumbani (NGOTORA), mila za kuabudu miungu, n.k, Ulanzi ndio huwa unatumika hasahasa kuliko pombe nyingine.
Kwahiyo,Wapangwa wote kama vile KINA WILLAH, HAULE, MULIGO, MTWEVE, NGAIRO, MWINUKA,n.k, ambao bado wanatii mila na desturi zao, Ulanzi kwao ni jadi.

CHANZO: Wikipedia

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...