Tuesday 14 April 2015

MAKALA: KUTOKANA NA KUKITHIRI KWA AJALI ZA BARABARANI, NINI KIFANYIKE?


PICHA: (Kwa hisani ya Tanzania today)

Wimbi la ajali limeendelea kuligubika taifa letu.Tumesikia na kusoma ajali mbali na za kusikitisha zilizotokea hivi karibuni. Hii ni hali ya kusikitisha sana kwani watu wasio na hatia wanapoteza maisha kutokana na uzembe wa mtu mmoja tu,DEREVA!
Watoto wengi wanabaki yatima na kuongeza idadi ya watoto wa mitaani, wanawake na wanaume wanabaki wajane, majeruhi wengi wanapata vilema vya maisha kutokana na uzembe wa huyu DEREVA!

Hebu angalia picha hii mazingira ambayo dereva wa basi anataka kulipita lori!Sijui leseni wamepewa na nani hawa!PICHA: (Kwa hisani ya Full Shangwe)

Hivi huyu  ni kweli DEREVA  yupo juu ya sheria?
Hivi kweli hakuna kinachoweza kufanyika ili kupunguza kama si kukomesha ajali hizi?Mimi binafsi nadhani kuna njia nyingi, zikiwemo za gharama nafuu na za gharama kubwa.


Tukianza na njia za gharama kubwa ni kutengeneza barabara zetu kuwa njia 2,yaani njia ya kwenda na njia ya kurudi. Hapa, hatutasikia tene ajali za kugongana uso kwa uso.
Ni gharama kujenga barabara hizi lakini inawezekana maana kuna pesa nyingi inatumika ndivyo sivyo na sina haja haja kuuelezea sana kuhusu hili kwani natumaini kuwa kila mmoja wetu anajua.
Njia ya pili ambayo haina gharama kabisa ni kuwafungia/kunyang´anya leseni madereva wote wanaosababisha ajali pamoja na kupewa adhabu ikiwemo za kifungo na kulipa mali aliyoharibu.
PICHA: (Kwa hisani ya Habarika blog)

Dereva yeyote aliyefungiwa/kunyang´anywa leseni asije kupewa leseni tena katika maisha yake. Adhabu hizi zote ziende sambamba!
Hii itaweka heshima katika barabara zetu na kunusuru maisha ya watu wasio na hatia.
Je mdau, wewe una mawazo gani? Tafadhali changia ili tuokoe maisha ya watu wasio na hatia!

Imeandikwa na Anna Nindi

No comments:

Post a Comment

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...