Showing posts with label ELIMU. Show all posts
Showing posts with label ELIMU. Show all posts

Sunday, 3 November 2013

JE,KUNA ALIYESOMA HIVI VITABU?

IF THERE IS AN ARROW OF GOD IN THE RIVER BETWEEN,THINGS FALL APART, NO LONGER AT EASE! 
Hii ni sentensi ambayo ni majina ya vitabu vifuatavyo:




 Vitabu hivi vinapatikana wapi?

                                                                     

Friday, 11 October 2013

UZINDUZI WA KAMPENI YA "TUSOME TANZANIA" NA RAIS MSTAAFU BENJAMINI W. MKAPA MAKTABA YA MKOA LEO JIJINI DAR

 Rais Mstaafu Mhe. Benjamini William Mkapa ambaye pia ni mgeni rasmi akihutubia vijana mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya tusome Tanzania (Let us read Tanzania) aliyoizindua leo katika viwanja vya Makao Makuu ya Maktaba ya Mkoa jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya vijana walioshiriki uzinduzi wa Kampeni ya tusome Tanzania (Let us read Tanzania) wakifuatilia kwa makini hotuba toka kwa mgeni rasmi Mhe. Benjamini William Mkapa (hayupo pichani) leo katika viwanja vya Makao Makuu ya Maktaba ya Mkoa jijini Dar es Salaam.
 Mmoja wa wadau toka timu ya Let us read Tanzania akimpa maelezo juu ya vitabu mbalimbali viliyotungwa na waandishi mashuhuri ndani na nje ya nchi.
Rais Mstaafu Mhe. Benjamini William Mkapa ambaye pia ni mgeni rasmi akiwasomea hadithi mbalimbali na kuwauliza maswali mbalimbali watoto ambao ni wanafunzi toka shule mmbalimbali leo katika viwanja vya Makao Makuu ya Maktaba ya Mkoa jijini Dar es Salaam.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO.
====== ========  =======
RAIS MSTAAFU MHE. BENJAMINI WILLIAM MKAPA AZINDUA KAMPENI YA TUSOME TANZANIA (LET US READ TANZANIA CAMPAIGN).
Na Benedict Liwenga-Maelezo, Dar es Salaam.
11/10/2013.
RAIS Mstaafu Mhe. Benjamini William Mkapa amezindua rasmi Kampeni ya “Tusome Tanzania (Let’s read Tanzania Campaign) iliyoandaliwa na wadau mbalimbali nchini wenye lengo la kuwahamasisha vijana wa kitanzania kujijengea utamaduni wa kusoma vitabu mbalimbali.
Katika uzinduzi huo, Mhe. Mkapa ameipongeza kamati ya wadau waandaaji wa kampeni hiyo kwa kujitoa kwao katika kuhakikisha kuwa watoto wa shule ambao ndiyo taifa la kesho wanapata kujionea wenyewe na anatumaini kuwa watahamasika kupenda kujisomea kwa manufaa ya maisha yao.

Friday, 13 September 2013

DARASA LA KISWAHILI: NAHAU NA MISEMO YA KISWAHILI

Katika kukienzi kiswahili,tukumbushane nahau, methali na misemo ya kiswahili kwa wale wanajua.Tutakuwa tunaelimishana kuhusu mambo mbalimbali yahusuyo lugha yetu ya kiswahili.

  1. Chombo cha kuzama hakina usukani.
  2. Asiye kubali kushindwa si mshindani
  3. Cha mlevi huliwa na mgema
  4. Asifuye mvuwa imemnyea.
  5. Kitanda usicho kilala hujui kunguni wake
  6. Mwomba chumvi huombea chunguche
  7. Mwenye kuchinja hachelei kuchuna
  8. Ukuukuu wa kamba si upya wa ukambaa
  9. Udugu wa nazi hukutania chunguni
  10. Mtoto umleyavyo ndivyo akuavyo
  11. ........................
  12. ..........................
  13. ...............................
  • Je,unaweza kuandika maana ya methali hizi?
  • Unaweza kuendeleza methali nyingine?
KARIBU TUELIMISHANE KWA KUTUMA MAONI YAKO!

Tuesday, 20 August 2013

Serikali yaanza kutoa masomo ya elimu ya juu ya sayansi ya hali ya hewa nchini, itatolewa UDSM


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA UCHUKUZI
MAMLAKA YA HALI YA HEWA 


 Simu: +255 22 2460706-8...

Telefax: +255 22 2460735, 2460700 S.L.P. 3056,
Barua pepe: met@meteo.go.tz DAR ES SALAAM
Tovuti: www.meteo.go.tz

Unapojibu Tafadhali nakili:

Kumb. No.TMA/4060/6/7: 20 Agosti 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Serikali yaanza kutoa masomo ya elimu ya juu ya sayansi ya hali ya hewa nchini.

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kushirikiana na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kimefanikisha uanzishwaji wa masomo ya shahada ya kwanza ya sayansi ya hali ya hewa (Bsc. Meteorology) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kuanzia muhula wa masomo 2013/14. 

Tuesday, 13 August 2013

DK NDALINACHO ‘ACHANACHANA‘ UBORA WA ELIMU TANZANIA


Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Nchini (Necta), Dk Joyce Ndalichako 
Arusha: Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Nchini (Necta), Dk Joyce Ndalichako amesema karatasi za majibu ambazo wamekuwa wakizipata kutoka kwa wanafunzi zinaonyesha kuwa, watoto wengi wanahudhuria shuleni lakini hakuna wanachojifunza.
Dk Ndalichako aliyasema hayo jana jijini hapa alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa mabaraza ya mitihani ya Afrika, ambao umejikita kujadili suala la tathimini ya elimu kwa nchi za Afrika.

Wednesday, 7 August 2013

PICHA YA SIKU



Watoto hawa ingawa wanasomea nje na mvua na jua ni vyao bado wana uchu wa elimu.Je,kuna anae wakumbuka hawa watoto kweli?Jadili halafu chukua hatua.

Saturday, 27 July 2013

INASIKITISHA:SAFARI YA KUPATA ELIMU


Sylvia ni msichana wa miaka minane anaishi kijiji kimoja Tanzania, licha ya maisha yake amejitolea kupata elimu na kila siku hutembea kwa saa moja unusu kwenda shuleni. Yeye ni miongoni mwa wasichana waliobahatika kupata elimu Barani Afrika
Safari ya msichana huyu kisha inampeleka barabara kuu. Wakati mwingine kuna jua kali, vumbi nyingi. Msimu wa jua barabara hujaa mapote na inampa changamoto msichana huyu katika safari yake shuleni
Ikiwa msichana huyu hataki vumbi na matope ya barabara, huamua kupitia kwenye njia ya reli. Hata hivyo kuna hatari zake, treni huenda ikaamkanyanga. Wakati mwingine watoto wa shule wamekua wakitekwa nyara.

Tuesday, 23 July 2013

Top 20 for Top 10s: QS World University Rankings by Subject 2013


1
University of Cambridge

Number of top 10 appearances: 27
Number one in: Historylinguisticsmathematics.
Position in QS World University Rankings 2012/13: 2
Country: UK

2=
University of Oxford

Number of top 10 appearances: 23
Position in QS World University Rankings 2012/13: 5
Country: UK

2=
University of California, Berkeley

Number of top 10 appearances: 23
Position in QS World University Rankings 2012/13: 22
Country: US

4
Stanford University

Number of top 10 appearances: 22
Position in QS World University Rankings 2012/13: 15
Country: US

Monday, 29 April 2013

NINI CHIMBUKO LA AGUKO LA ELIMU TANZANIA?


Watoto wakiwa wamekalia ndoo


Watoto wakiwa wamebanana na wengine hawana meza ya kuandikia


Hapa sijui ni shule nzima au darasa moja


Moja ya shule katika bonde la Ngorongoro


Kunapokuwa na tatizo au mapungufu lazima kuna sababu iliyopelekea kuwepo tatizo hilo.Tatizo haliwezi kwisha bila kutibu/kurekebisha chanzo cha tatizo.

Je,nini kimechangia la anguko la elimu Tanzania?Je,sababu zinaweza kuwa:
Ubadilishwaji wa mitaala mara kwa mara
Ubadilishwaji wa vitabu bila kufuata utaratibu
Mrundikano wa watoto darasani
Ukosefu wa madawati
Majengo duni
Maslahi duni ya walimu
Wadau mnaweza kuchangia ili kusaidia uboreshaji wa elimu yetu.

PALM TREES ARE BEAUTIFUL

Minazi huleta mandhari nzuri ya kuvutia, haijalishi ni sehemu gani imemea. Palm trees are always beautiful, it doesn´t matter where they are...